Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

“Mnapaswa kuwa walimu.” (Ebr. 5:12) Hebu wazia! Yehova—yule Mwalimu bora zaidi ulimwenguni—anatualika sisi tuwafundishe wengine kumhusu! Mgawo wowote wa kufundisha kweli kumhusu Yehova—iwe ni katika familia, katika kutaniko, au katika huduma ya shambani—ni pendeleo kubwa na daraka zito. Tunaweza kufanya nini ili tufaulu?

Jibu linapatikana katika maneno ambayo mtume Paulo alimwandikia Timotheo: “Endelea kujitahidi kusoma mbele ya watu, kuhimiza, na kufundisha.” Paulo aliongezea kusema: “Ukifanya hivyo utajiokoa wewe mwenyewe na wale wanaokusikiliza pia.” (1 Tim. 4:13, 16) Umepewa ujumbe unaoweza kuokoa uhai. Kwa hiyo, ni muhimu sana uendelee kuboresha usomaji na ufundishaji wako. Broshua hii imekusudiwa kukusaidia kufanya hivyo. Hebu chunguza baadhi ya mambo yaliyomo.

Katika kila ukurasa kuna andiko ambalo linatoa kanuni ya Biblia inayohusiana na somo linalozungumziwa au linaloonyesha jinsi somo hilo linavyoweza kutumiwa

Yehova ndiye ‘Mfundishaji Mkuu.’ (Isa. 30:20) Ingawa broshua hii itakusaidia kuboresha ustadi wako wa kusoma na kufundisha, usisahau kamwe kwamba Yehova ndiye Chanzo cha ujumbe tunaowasilisha na ndiye anayewavuta watu. (Yoh. 6:44) Kwa hiyo, sali mara nyingi upate roho takatifu. Litumie Neno la Mungu mara nyingi. Usijielekezee fikira kamwe, bali sikuzote mwelekezee Yehova sifa. Jitahidi kuwasaidia wasikilizaji wako wampende Yehova sana.

Umepewa mgawo wa kufundisha ujumbe muhimu zaidi ambao wanadamu wamewahi kupewa. Tuna uhakika kwamba ukitegemea “nguvu ambazo Mungu hutoa,” utafanikiwa.​—1 Pet. 4:11.

Walimu wenzako,

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova