Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Fahirisi ya Picha

Fahirisi ya Picha

Zikirejelewa Kulingana Na Kurasa

  • Majalada Paulo, Tabitha, Galio, Luka, ofisa wa hekaluni pamoja na mitume, Sadukayo, Paulo akipelekwa Kaisaria, mahubiri katika siku zetu na gari lenye vikuza sauti na kinanda cha gramafoni.

  • Ukurasa wa 1 Paulo amefungwa minyororo, akiwa na Luka katika meli yenye shehena inayoelekea Roma.

  • Ukurasa wa 2, 3 Ndugu J. E. Barr na T. Jaracz wa Baraza Linaloongoza wakiangalia ramani ya dunia.

  • Ukurasa wa 11 Yesu akiwa kwenye mlima wa Galilaya, anawatuma wale mitume 11 waaminifu na wafuasi wengine.

  • Ukurasa wa 14 Yesu anapaa kwenda mbinguni huku mitume wakimtazama.

  • Ukurasa wa 20 Siku ya Pentekoste, wanafunzi waanza kuzungumza na wageni katika lugha zao wenyewe.

  • Ukurasa wa 36 Mitume wamesimama mbele za Kayafa mwenye hasira. Sanhedrini yawatuma maofisa wa hekalu wakawakamate mitume.

  • Ukurasa wa 44 Chini: Baada ya Vita vya Pili vya Ulimwengu, mahakama ya Ujerumani Mashariki yawahukumu kimakosa Mashahidi wa Yehova kuwa wapelelezi wa Marekani.​—Jarida la Neue Berliner Illustrierte, la Oktoba 3, 1950.

  • Ukurasa wa 46 Stefano akiwa mbele ya Sanhedrini. Masadukayo matajiri wakiwa wameketi upande wa kushoto wa Stefano, nao Mafarisayo wenye kushikilia mambo kupita kiasi wakiwa wameketi upande wake wa kulia.

  • Ukurasa wa 54 Petro aweka mikono yake juu ya mwanafunzi mpya; Simoni akiwa amebeba mfuko wa sarafu.

  • Ukurasa wa 75 Petro na wenzake waingia nyumbani kwa Kornelio. Kornelio amevaa vazi la pekee kwenye bega lake la kushoto kuonyesha cheo chake akiwa ofisa wa jeshi.

  • Ukurasa wa 83 Petro aongozwa na malaika; huenda Petro alifungwa katika gereza la Mnara wa Antonia.

  • Ukurasa wa 84 Chini: Umati wa watu wenye vurugu karibu na Montreal, Quebec, mwaka wa 1945.​—Jarida la Weekend Magazine, la Julai 1956.

  • Ukurasa wa 91 Paulo na Barnaba watupwa nje ya jiji la Antiokia ya Pisidia. Mfereji mpya wa maji wa jiji hilo, ambao huenda ulijengwa katika karne ya kwanza W.K., waonekana sehemu ya nyuma.

  • Ukurasa wa 94 Paulo na Barnaba wakataa kusifiwa jijini Listra. Kwa kawaida, pindi za kutoa dhabihu zilikuwa pindi zenye shangwe, shamrashamra na muziki.

  • Ukurasa wa 100 Juu: Sila na Yuda wakitia moyo kutaniko la Antiokia ya Siria. (Mdo. 15:30-32) Chini: Mwangalizi wa mzunguko akitoa hotuba katika kutaniko nchini Uganda.

  • Ukurasa wa 107 Kutaniko la Yerusalemu lakutana katika nyumba ya mwabudu mwenzao.

  • Ukurasa wa 124 Paulo na Timotheo wakisafiri katika meli ya biashara ya Roma. Mnara wa taa waonekana kwa mbali.

  • Ukurasa wa 139 Paulo na Sila wakiwa kwenye mlango uliofungwa, wakikimbia umati wenye hasira.

  • Ukurasa wa 155 Galio akiwakemea wanaomshtaki Paulo. Amevaa vazi linalofaa cheo chake: nguo nyeupe ya kifalme yenye upindo wa zambarau na viatu vinavyoitwa calcei.

  • Ukurasa wa 158 Demetrio akizungumza na mafundi katika duka la fedha jijini Efeso. Vihekalu vya fedha vya Artemi huuzwa kama bidhaa za kumbukumbu.

  • Ukurasa wa 171 Paulo na wenzake wapanda meli. Nguzo Kuu ya Bandari, iliyojengwa katika karne ya kwanza K.W.K., yaonekana sehemu ya juu upande wa kulia.

  • Ukurasa wa 180 Chini: Miaka ya 1940 hivi, wakati ambapo vitabu na magazeti yetu yalipigwa marufuku nchini Kanada, kijana Shahidi akiingiza kisiri vitabu na magazeti ya Biblia. (Igizo.)

  • Ukurasa wa 182 Paulo akubali ombi la wazee. Luka na Timotheo wameketi sehemu ya nyuma wakisaidia kuwasilisha michango.

  • Ukurasa wa 190 Mpwa wa Paulo azungumza na Klaudio Lisia katika Mnara wa Antonia, ambapo huenda Paulo alikuwa amefungiwa. Hekalu la Herode linaonekana kupitia dirishani.

  • Ukurasa wa 206 Paulo anasali kwa ajili ya wasafiri waliochoka katika sehemu ya mizigo ya meli.

  • Ukurasa wa 222 Mfungwa Paulo, akiwa amefungwa mnyororo pamoja na askari Mroma, akitazama sehemu ya jiji la Roma.