Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Umalizio

Umalizio

Je, kuna nyakati ambazo wewe hukumbuka pindi nzuri ulizofurahia pamoja na watu wa Yehova, iwe ni mkutano wa kutaniko wenye kutia moyo, kusanyiko lenye kuchochea, jambo lililoonwa katika utumishi wa shambani, au mazungumzo yenye kupendeza pamoja na mwamini mwenzako? Hujamsahau Yehova; naye pia hajakusahau. Anakumbuka na kuthamini utumishi wako mwaminifu. Naye yuko tayari kukusaidia ili umrudie.

Yehova anasema hivi: “Nami nitawatafuta kondoo zangu na kuwatunza. Kulingana na utunzaji wa mtu anayelisha kundi lake katika siku ya kuja kwake kuwa katikati ya kondoo zake ambao wametawanyika kotekote, hivyo ndivyo nitakavyowatunza kondoo zangu; nami nitawakomboa kutoka mahali pote ambapo wametawanyika.”—Ezekieli 34:11, 12.