Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 10

Wanaomsikiliza Mungu Watapata Baraka Gani?

Wanaomsikiliza Mungu Watapata Baraka Gani?

Watu wengi ambao wamekufa watafufuliwa waishi duniani. Matendo 24:15

Wazia baraka utakazofurahia wakati ujao ikiwa utamsikiliza Yehova! Utakuwa na afya kamilifu; hakuna mtu atakayekuwa mgonjwa au dhaifu. Watu wabaya hawatakuwako, nawe utaweza kumwamini kila mtu.

Hakutakuwa na maumivu, huzuni, au machozi. Hakuna mtu atakayezeeka na kufa.

Utazungukwa na marafiki na watu wa familia. Maisha katika Paradiso yatafurahisha sana.

Hakutakuwa na woga. Watu watakuwa wenye furaha kwelikweli.

Ufalme wa Mungu utaondoa mateso yote. Ufunuo 21:3, 4