Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 9

Dunia Itakuwa Paradiso Wakati Gani?

Dunia Itakuwa Paradiso Wakati Gani?

Matatizo yaliyo duniani yanathibitisha kwamba hivi karibuni Ufalme wa Mungu utaleta mabadiliko. Luka 21:10, 11; 2 Timotheo 3:1-5

Biblia ilitabiri kuhusu mambo mengi yanayotukia leo. Ilisema kwamba watu wangekuwa wenye kupenda pesa, wasiotii wazazi, wakali, na wanaopenda raha.

Kungekuwa na matetemeko makubwa ya ardhi, vita, upungufu wa chakula, na magonjwa yangeenea. Mambo hayo yanatukia sasa.

Pia, Yesu alisema kwamba habari njema ya Ufalme ingehubiriwa katika dunia yote.—Mathayo 24:14.

Ufalme utaondoa uovu wote. 2 Petro 3:13

Yehova atawaharibu waovu wote hivi karibuni.

Shetani na roho waovu wataadhibiwa.

Watu wanaomsikiliza Mungu wataokoka na kuingia katika ulimwengu mpya wenye uadilifu, ambako hakutakuwa na hofu, na watu watapendana na kuaminiana.