Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 11

Je, Yehova Hutusikiliza?

Je, Yehova Hutusikiliza?

Mungu husikiliza sala zetu. 1 Petro 3:12

Yehova ni ‘Msikiaji wa sala.’ (Zaburi 65:2) Anataka tuzungumze naye kutoka moyoni.

Sali kwa Yehova, na si kwa mwingine yeyote.

Kuna mambo mengi tunayoweza kutaja katika sala. 1 Yohana 5:14

Sali mapenzi ya Mungu yatendeke mbinguni na duniani.

Sali katika jina la Yesu ili kuonyesha kwamba unathamini mambo aliyokufanyia.

Mwombe Yehova akusaidie kufanya mema. Unaweza pia kusali kuhusu chakula, kazi, makao, mavazi, na afya.