Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 1

Tunamsikiliza Mungu Jinsi Gani?

Tunamsikiliza Mungu Jinsi Gani?

Mungu anazungumza nasi kupitia Biblia. 2 Timotheo 3:16

Mungu wa kweli aliwaongoza wanaume fulani kuandika mawazo yake katika kitabu kimoja kitakatifu. Kitabu hicho ni Biblia. Biblia ina habari muhimu ambazo Mungu anataka uzijue.

Mungu anajua mambo yanayotufaa zaidi, na yeye ndiye Chanzo cha hekima yote. Ukimsikiliza, utapata hekima ya kweli.—Methali 1:5.

Mungu anataka kila mtu duniani asome Biblia. Inapatikana katika lugha nyingi leo.

Ikiwa unataka kumsikiliza Mungu, ni lazima usome Biblia na kuielewa.

Watu kila mahali wanamsikiliza Mungu. Mathayo 28:19

Mashahidi wa Yehova wanaweza kukusaidia uielewe Biblia.

Wanafundisha ukweli kumhusu Mungu duniani pote.

Huhitaji kulipa chochote ili ufundishwe. Unaweza pia kujifunza kumhusu Mungu katika Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova lililo karibu na mahali unapoishi.