Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Ile Dunia-Paradiso

Ile Dunia-Paradiso

Yehova ataondolea mbali mambo yote mabaya ambayo Shetani amefanya. Yehova amemweka Yesu kuwa Mfalme juu ya dunia yote. Chini ya utawala wake, dunia itafanywa kuwa paradiso.—Danieli 7:13, 14; Luka 23:43.

Yehova anaahidi mambo haya:

  • KUTAKUWA NA CHAKULA TELE: “Dunia itatoa mazao yake; Mungu, Mungu wetu, atatubariki.” “Kutakuwa na nafaka nyingi duniani; itafurika juu ya milima.”—Zaburi 67:6; 72:16.

  • VITA HAVITAKUWAPO TENA: “Njooni mtazame matendo ya Yehova, jinsi alivyotenda mambo yanayostaajabisha duniani. Anakomesha vita katika dunia yote.”—Zaburi 46:8, 9.

  • WATU WABAYA HAWATAKUWAPO TENA: “Kwa maana waovu wataangamizwa . . . Bado muda mfupi tu, na watu waovu hawatakuwepo tena; utapaangalia mahali walipokuwa, nao hawatakuwepo.”—Zaburi 37:9, 10.

  • MAGONJWA, HUZUNI, NA KIFO HAVITAKUWAPO TENA: “Wakati huo macho ya vipofu yatafunguliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa. Wakati huo kilema ataruka kama paa, na ulimi wa bubu utapiga vigelegele vya shangwe.”—Isaya 35:5, 6.

    “Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. Naye atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”—Ufunuo 21:3, 4.

Tofauti na Shetani na roho wake waovu, Yehova hasemi uwongo kamwe. Kila kitu anachoahidi kitatimia. (Luka 1:36, 37) Yehova anakupenda na anataka uishi katika Paradiso atakayoifanya. Kwa hiyo wasiliana na Mashahidi wa Yehova ili ujifunze mengi zaidi kuhusu kweli hizi nzuri ajabu zinazopatikana katika Neno la Mungu. Ukiitumia kweli katika maisha yako, utawekwa huru kutokana na utumwa wa uwongo na ushirikina. Kisha utafunguliwa kutoka katika utumwa wa dhambi na kifo. Kama alivyosema Yesu: ‘Utaijua kweli, nayo kweli itakuweka huru.’—Yohana 8:32.