Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wakati Ujao Mzuri Ajabu

Wakati Ujao Mzuri Ajabu

Karibuni Shetani na roho wake waovu watafungwa

Shetani na roho wake waovu hawatawadanganya wanadamu kwa muda mrefu. Tayari Yehova amewatupa kutoka mbinguni. (Ufunuo 12:9) Hivi karibuni, Mungu atachukua hatua tena dhidi ya Shetani na roho wake waovu. Katika maono kutoka kwa Mungu, mtume Yohana alisema hivi: “Nikamwona malaika akishuka kutoka mbinguni akiwa na ufunguo wa shimo refu lisilo na mwisho na mnyororo mkubwa mkononi mwake. Akamkamata yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, na kumfunga kwa miaka 1,000. Naye akamtupa katika shimo refu lisilo na mwisho akalifunga na kulitia muhuri juu yake, ili asipotoshe mataifa tena mpaka ile miaka 1,000 itakapokwisha.” (Ufunuo 20:1-3) Baadaye, Ibilisi na roho wake waovu wataangamizwa milele.—Ufunuo 20:10.

Watu wabaya duniani wataangamizwa pia.—Zaburi 37:9, 10; Luka 13:5.

Wafu Wataishi Tena!

Wafu watafufuliwa waishi tena duniani

Baada ya Shetani na roho wake waovu kuondolewa, Yehova atawaletea wanadamu baraka nyingi. Kumbuka kwamba wafu hawako hai, hawapo popote. Yesu alilinganisha kifo na usingizi—usingizi mzito usio na ndoto. (Yohana 11:11-14) Alifanya hivyo kwa sababu alijua kwamba wakati ungefika ambapo wale wanaolala katika kifo wangeamshwa waishi tena. Alisema: ‘Saa inakuja ambayo wote walio katika makaburi ya ukumbusho watatoka.’—Yohana 5:28, 29; Linganisha Matendo 24:15.

Watafufuliwa waishi hapa duniani. Badala ya matangazo ya vifo, kutakuwa na ripoti zenye kufurahisha za wale ambao wamefufuliwa! Itakuwa shangwe kama nini kuwakaribisha wapendwa wetu kutoka kaburini!