Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, unatamani kuona ahadi za Ufalme zikitimia?

SEHEMU YA 7

Ahadi za Ufalme​—Kufanya Vitu Vyote Kuwa Vipya

Ahadi za Ufalme​—Kufanya Vitu Vyote Kuwa Vipya

UNACHUMA tofaa kubwa lililoiva. Unanusa harufu yake nzuri kabla ya kuweka kwenye kikapu chako kilichojaa matunda. Umekuwa ukifanya kazi kwa saa nyingi, lakini hujachoka na uko tayari kufanya kazi nyingine zaidi. Mama yako yuko karibu na mti fulani, akifurahia kazi na mazungumzo pamoja watu wengine wa familia na marafiki ambao wanasaidia kuvuna. Anaonekana akiwa kijana sana—kama alivyokuwa wakati wa miaka yako yote ya utotoni. Uliumia sana ulipomwona mama yako akizeeka katika ulimwengu ambao sasa umepitilia mbali miaka mingi iliyopita. Ulimwona akiwa amedhoofishwa na ugonjwa, uliushika mkono wake alipokuwa akikata pumzi, na ukalia kwa uchungu sana juu ya kaburi lake. Hata hivyo, mama yako pamoja na watu wengine wengi sana wako hai tena na wenye afya bora.

Tunajua kwamba siku hizo zitakuja. Tunajua hivyo kwa sababu ahadi za Mungu sikuzote hutimia. Katika sehemu hii, tutachunguza jinsi ambavyo baadhi ya ahadi za Ufalme zitatimizwa hivi karibuni, katika kipindi kinachoongoza kwenye vita vya Har–Magedoni. Pia tutachunguza ahadi zenye kusisimua za Ufalme ambazo zitatimizwa baadaye. Tutafurahia kwelikweli kuona wakati ambapo Ufalme wa Mungu unatawala dunia hii nzima na kufanya vitu vyote kuwa vipya!

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 21

Ufalme wa Mungu Unaondoa Maadui Wake

Unaweza kujitayarisha sasa kwa ajili ya vita vya Har–​Magedoni.

SURA YA 22

Ufalme Unatimiza Mapenzi ya Mungu Duniani

Unawezaje kuwa na uhakika kwamba ahadi za Yehova zitatimia?