Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kushoto: Dada kolpota akihubiri nchini Korea, 1931; Kushoto: Dada kolpota akihubiri nchini Korea, 1931

SEHEMU YA 2

Kuhubiri Kuhusu Ufalme​—Kutangaza Habari Njema Ulimwenguni Pote

Kuhubiri Kuhusu Ufalme​—Kutangaza Habari Njema Ulimwenguni Pote

ASUBUHI na mapema, siku ya mapumziko unajitayarisha kwa ajili ya utumishi wa shambani. Unasita kwa muda kwa kuwa unahisi uchovu kidogo. Unatamani kuendelea kupumzika! Hata hivyo, unasali kuhusu jambo hilo na unaazimia kwenda. Unahubiri na dada mzee ambaye amekuwa mwaminifu kwa muda mrefu, na uvumilivu na fadhili zake zinagusa moyo wako. Na unapohubiri ujumbe wa ile kweli nyumba kwa nyumba, unakumbuka kwamba ndugu na dada zako ulimwenguni pote wanahubiri ujumbe huohuo, wakitumia machapisho yaleyale, na kunufaika na mazoezi yaleyale ambayo umepata. Unaporudi nyumbani, unahisi umetiwa nguvu. Unafurahi sana kwamba hukukaa nyumbani!

Leo, huduma ya Kikristo ndiyo kazi kuu ya Ufalme wa Mungu. Yesu alitabiri kwamba kazi ya kuhubiri itafanywa kwa kiwango kikubwa katika siku za mwisho. (Mt. 24:14) Unabii wake umetimizwa jinsi gani? Katika sehemu hii, tutachunguza watu, mbinu, na vifaa ambavyo vimekuwa muhimu sana katika huduma ya Kikristo, ambayo inawasaidia mamilioni ya watu ulimwenguni pote kuona kwamba Ufalme wa Mungu ni halisi.

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 6

Watu Wanaohubiri​—Wahudumu Wanajitoa kwa Hiari

Kwa nini Yesu alikuwa na uhakika kwamba angekuwa na jeshi la watu wanaohubiri kwa hiari katika siku za mwisho? Unaweza kuonyeshaje kwamba unautafuta kwanza Ufalme?

SURA YA 7

Mbinu za Kuhubiri​—Kutumia Kila Njia Ili Kuwafikia Watu

Soma kuhusu mbinu ambazo watu wa Mungu wametumia kuwafikikishia habari njema watu wengi kadiri iwezekanavyo kabla ya mwisho kuja.

SURA YA 8

Vifaa vya Kutusaidia Kuhubiri​—Kuchapisha Machapisho kwa Ajili ya Watu Ulimwenguni Pote

Kazi yetu ya kutafsiri inathibitishaje kwamba tunaungwa mkono na Yesu? Ni mambo gani ya hakika kuhusu machapisho yetu yanayokuthibitishia kwamba Ufalme ni halisi?

SURA YA 9

Matokeo ya Kuhubiri​—“Mashamba . . . Ni Meupe kwa Ajili ya Kuvunwa”

Yesu aliwafundisha wanafunzi wake mambo mawili muhimu kuhusu mavuno makubwa zaidi ya kiroho. Mambo hayo mawili yanatuathiri jinsi gani leo?