Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Ulimwengu Usio na Vita​—Wewe Waweza Kuuona

Ulimwengu Usio na Vita​—Wewe Waweza Kuuona

1-4. (a) Kwa nini huu ni wakati wa haraka kufanya uamuzi? (b) Ikiwa mtu atafanya uamuzi ufaao ni jambo gani linalotakwa lifanywe?

ULE unabii wenye kuchochea wa Isaya sura ya 2 unatimia kweli kweli katika siku zetu. Ulimwengu usio na vita u karibu. Tayari mamilioni ya Mashahidi wa Yehova kuzunguka dunia wamefua “panga zao ziwe majembe ya plau na mikuki yao iwe miundu ya kupogolea.” Ijapokuwa watoka katika kila taifa na malezi, wamejifunza kushinda hasama na chuki za zamani, nao wamejifunza njia za Mungu wa amani ya kweli, Yehova. (Isaya 2:4) Kwa sababu ya msimamo huo wenye kupenda amani, walishiriki yaliyowapata Wayahudi katika kambi za mateso (1933-45).

2 Hata matarajio ya wakati ujao yawe mazuri kama yalivyo, si mazuri kwa wote. Yehova hatangoja kwa wakati usio na mwisho ili wanadamu wote wafue panga zao kuwa majembe ya plau. Kuna wale wasiotaka kufanya hivyo. Mtunga zaburi haachi shaka kwa habari ya yatakayowapata hao: “Maana watu waovu watakatiliwa mbali, bali wale ambao humtazamia BWANA—watairithi nchi. Bado kitambo kidogo na mtu mwovu hatakuwako; utatazama mahali alipokuwa—atakuwa ameenda.” (Zaburi 37:9, 10) Naam, katika wakati ujao ulio karibu, Yehova atachukua hatua, ‘akikomesha vita kotekote duniani.’​—Zaburi 46:9-11 (46:8-10, UV).

3 Unabii uleule wa Yesu uliotoa ishara ya siku za mwisho ulikazia pia ukaribu wa kujiingiza kwa Mungu katika mambo ya wanadamu. Yesu alisema: “Kizazi hiki [kile kizazi cha 1914 ambacho kilishuhudia mwisho wa “zile nyakati zilizowekwa za mataifa”] hakitapita kamwe hata mambo haya yote yatukie.” (Mathayo 24:34; Luka 21:24, NW) Kizazi hicho chakaribia sana kupitilia mbali. Ndiyo, sasa ndio wakati wa uamuzi kwa ainabinadamu yote! Sasa, katika siku hizi za mwisho, au “mwisho wa siku,” (JP) ni lazima sisi tuchague kama ‘tutapanda kwenda kwenye mlima wa Yehova’ ‘tukafunzwe katika njia Zake’ au la. Lakini kama vile tumeona kutokana na mazungumzo haya, mengi zaidi yahusika katika kuja kumjua Mungu wa kweli, ‘katika kufunzwa katika njia Zake, katika kutembea katika vijia Vyake.’ (Isaya 2:2, 3, NW, Ta) Kufanya hivyo si jambo tu la kusoma broshua hii au kuchukua mtaala mfupi wa funzo. Yahusu kufunzwa kwenye kina kirefu zaidi kunakoathiri njia yote ya maisha ya mtu. Je! wewe ungependa kujua zaidi juu ya Mungu wa amani?

4 Mashahidi wa Yehova wako tayari kukusaidia ufanye uchunguzi mzito kama huo. Twakutia moyo uendelee kuchunguza habari hii kwa bidii yote ya moyo, ili wewe pia uweze kuwa miongoni mwa wale ‘wapandao kwenda kwenye mlima wa Yehova, wafunzwao katika vijia Vyake.’ Ili kupata msaada zaidi, onana na Mashahidi wa Yehova kwenye Jumba la Ufalme au ofisi ya tawi iliyo karibu nawe, Matokeo yenye kuridhisha yanaelezwa vizuri na nabii Mika: “Nao kwa kweli wataketi, kila mmoja chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, na hapatakuwa na yeyote wa kuwafanya wateteme.” Wewe na uwe miongoni mwa wale ambao ‘hutembea katika jina la Yehova milele’ katika ulimwengu usio na vita!—Mika 4:4, 5NW.