Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Utangulizi

Utangulizi

Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?​—Katika wakati wetu tumeona vita vyenye kuangamiza zaidi vilivyopata kutaabisha ainakibinadamu. Mamilioni ya wajane wa kiume na wa kike, na mayatima wameachwa waombolezee wapendwa wao. Kwenye mashauriano ya amani ya 1991 katika Madrid, kule Mashariki ya Kati, Yitzhak Shamir alisema hivi: “Mimi nina hakika kwamba hakuna mama Mwarabu atakaye mwana wake afe katika pigano​—kama vile hakuna mama Myahudi atakaye mwana wake afe katika vita.” Hivyo, kichwa chetu kinafaa, Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?

Pia, umepata kuuliza: Je! kuna njia yoyote ya kuthibitisha kuwako kwa Mungu? Ikiwa ipo, kwa nini ameruhusu kuteseka kwingi sana? Kusudi la Mungu ni nini kwetu na sisi, twaweza kulijuaje? Kuna uthibitisho gani kwamba Biblia imepuliziwa na Mungu? Ni nini iliyo hali ya wafu, na kuna tumaini gani kwao, likiwako lolote? Maswali hayo na mengine yatazungumziwa wakati wa mazungumzo haya.

Ml. Hermoni

Bahari ya Galilaya

Ml. Tabori

Dunia ingekuwa paradiso lakini mwanadamu ameifanya kuwa uwanja wa vita