Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 14

Ufalme Ambao Utatawala Dunia Nzima

Ufalme Ambao Utatawala Dunia Nzima

Je, unaweza kukisia ni Ufalme gani huo?— Bila shaka, ni Ufalme wa Mungu, Ufalme ambao utaifanya dunia nzima iwe paradiso. Je, ungependa kujifunza mambo fulani kuhusu Ufalme huo?—

Kila ufalme una mfalme. Na mfalme huwatawala watu walio chini ya utawala wake. Je, unajua jina la Mfalme wa Ufalme wa Mungu?— Jina lake ni Yesu Kristo. Anaishi mbinguni. Hivi karibuni atakuwa Mfalme juu ya dunia nzima! Je, unafikiri tutakuwa na furaha Yesu atakapoitawala dunia nzima?—

Utafurahia mambo gani katika Paradiso?

Tutafurahi sana! Katika Paradiso, watu hawatagombana tena wala kwenda vitani. Watu wote watapendana. Hakuna mtu atakayekuwa mgonjwa au kufa. Vipofu wataona, viziwi watasikia, na wale ambao hawawezi kutembea watakimbia na kuruka. Kila mtu atakuwa na chakula cha kutosha. Wanyama wataishi pamoja bila kuumizana, na pia wanadamu wataishi kwa amani pamoja na wanyama. Watu ambao wamekufa watafufuliwa. Wanaume na wanawake wengi ambao umejifunza kuwahusu katika broshua hii, kama vile Rebeka, Rahabu, Daudi, na Eliya watafufuliwa pia! Je, ungependa kukutana nao watakapofufuliwa?—

Yehova anakupenda na anataka uwe na furaha. Ukiendelea kujifunza kuhusu Yehova na kumtii, utaweza kuishi milele katika paradiso nzuri sana! Je, ungependa kuishi katika paradiso hiyo?—