Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

NYONGEZA B

Je, Usitishe Mazungumzo?

Je, Usitishe Mazungumzo?

Sisi hufurahia kuendeleza mazungumzo na mtu anayeuliza swali kwa unyofu au anayeomba tufafanue jambo fulani. Tunataka kuzungumza na watu ambao huenda wana “mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele.”—Mdo. 13:48.

Lakini inakuwaje ikiwa mtu ana hasira, anataka tubishane, au hataki kuzungumza wakati huo? Sitisha mazungumzo hayo kwa utulivu na fadhili. (Met. 17:14) Jitahidi kumaliza mazungumzo kwa amani, ili mtu huyo aweze kuwa tayari kuzungumza nasi wakati ujao.—1 Pet. 2:12.