KUFANYA WANAFUNZI
SOMO LA 11
Fundisha kwa Njia Rahisi
Kanuni: ‘Sema maneno yanayoeleweka kwa urahisi.’ —1 Kor. 14:9.
Yesu Alifanya Nini?
1. Tazama VIDEO, au soma Mathayo 6:25-27. Kisha fikiria maswali yafuatayo:
Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?
2. Tunapofundisha kwa njia rahisi, watu watakumbuka mambo tunayowafundisha na tutagusa mioyo yao.
Mwige Yesu
3. Usizungumze kupita kiasi. Badala ya kuzungumzia kila kitu unachojua kuhusu somo hilo, kazia habari zilizo katika chapisho mnalojifunza. Baada ya kuuliza swali, subiri mwanafunzi wako atoe jibu. Ikiwa hajui jibu au anasema jambo lisilopatana na mafundisho ya Biblia, tumia maswali ya ziada kumsaidia aelewe habari hiyo. Mwanafunzi wako anapoelewa jambo kuu, endelea na sehemu inayofuata.
4. Msaidie mwanafunzi wako aone jinsi mafundisho mapya yanavyohusiana na mambo anayojua. Kwa mfano, kabla ya kuanza kujifunza kuhusu ufufuo, mnaweza kurudia kwa ufupi mambo ambayo mwanafunzi wako amejifunza kuhusu hali ya wafu.
5. Tumia mifano kwa uangalifu. Kabla ya kutumia mfano, jiulize hivi: