Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

TOVUTI YA JW.ORG

Tumia Biblia ya Kujifunzia

Tumia Biblia ya Kujifunzia

Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya (Toleo la Funzo) ina sehemu mbalimbali za kujifunzia, zinazotia ndani mambo yafuatayo:

  • Utangulizi wa kila kitabu cha Biblia, ambao unaweza kutia ndani video ya utangulizi

  • Mambo makuu, au muhtasari, wa kila kitabu cha Biblia

  • Habari za utafiti za mstari wa Biblia

  • Maelezo ya chini ya maneno au semi

  • Marejeo ya pambizoni

  • Picha na video

  • Nyongeza zenye ramani, michoro, na habari za utafiti

  • Rekodi za sauti za usomaji wa kila sura

  • Tafsiri za mstari huo katika Biblia nyingine

Toleo la funzo la kitabu cha Mathayo kilitolewa katika Kiingereza mwezi wa Oktoba 2015. Mambo mengi yameongezewa kwenye habari za utafiti za vitabu mbalimbali vilivyokamilishwa.

Jifunze kutumia sehemu hii ya Biblia ya Kujifunzia:

 Fungua kitabu cha Biblia na sura

Tafuta kwenye MAKTABA >BIBLIA YA MTANDAONI kisha teua bofya Bibilia Takatifu-Tafsiri ya Ulimwengu Mpya (toleo la funzo la Kiingereza) jalada au kiunganishi ili kufungua sehemu ya Yaliyomo.

  • Alama ya almasi inaonyesha kwamba habari za kujifunzia za kitabu hicho cha Biblia zinapatikana.

  • Alama ya kifaa cha kusikiliza inaonyesha kwamba rekodi ya sauti ya kitabu hicho inapatikana.

  • Bofya sehemu ya Mpangilio wa Mraba kufungua mpangilio wa kawaida wa vitabu vya Biblia ya Kujifunzia.

  • Bofya sehemu ya Orodha kufungua mpangilio wa wima wa vitabu vya Biblia ya Kujifunzia, ulio na orodha ya Maandiko ya Kiebrania-Kiaramu na ya Kigiriki ya Kikristo katika safu mbili tofauti.

Kuna viunganishi kwa ajili ya habari nyingi za ziada, kutia ndani kamusi ya maneno, nyongeza, picha na video.

Tumia njia moja kati ya njia zifuatazo ili kufungua kitabu na sura fulani katika Biblia.

Njia ya 1: Chagua kitabu cha Biblia katika ukurasa wenye Yaliyomo. Ukurasa utakaofunguka utatia ndani orodha ya sura za kitabu hicho, mambo makuu ya kitabu, na alama za sehemu nyingine za Biblia hii:

  • Utangulizi wa kitabu hicho cha Biblia, unaotia ndani video ya utangulizi ikiwa inapatikana.

  • Mambo makuu ya kitabu hicho cha Biblia.

  • Sehemu ya picha na video zinazohusiana na kitabu hicho cha Biblia.

Fungua sura unayotaka kujifunza.

Njia ya 2: Tumia sehemu ya juu ya ukurasa huo ili kuchagua kitabu na sura fulani katika Biblia.

 Tumia vifaa vya kujifunzia vya sura ya Biblia

Upande wa kushoto kuna Maandiko ya Biblia ya sura husika na upande wa kulia kuna Habari za Utafiti. Katika vifaa vya mkononi, safu ya Habari za Utafiti hujitokeza unapofungua mstari wa Biblia, alama za maelezo ya chini, au herufi za marejeo.

  • Bofya sura au namba ya mstari, ili kufungua habari za utafiti za mstari huo.

  • Bofya alama ya maelezo ya chini kupata ufafanuzi wa neno au semi.

  • Bofya herufi za marejeo ya pambizoni kupata marejeo zaidi katika safu ya Habari za Utafiti na mistari mingine ya Biblia.

  • Ili kucheza rekodi ya sauti ya sura fulani ukianzia mstari fulani hususa, bofya maneno ya mstari huo, kisha bofya alama ya Kucheza.

  • Ili kucheza rekodi ya sauti ya sura fulani ukianzia mwanzo, bofya alama ya Cheza iliyo juu ya ukurasa.

  • Ili kukatiza rekodi ya sauti isiendelee, bofya alama ya Tua iliyo mwanzoni mwa ukurasa kwenye kisanduku cha rekodi.

  • Bofya alama ya Hazina katika safu ya Habari za Utafiti ili kupata habari zote za utafiti, maelezo ya chini, marejeo ya pambizoni, picha na video ya sura hiyo. (Ukurasa wa Hazina hufunguka wenyewe unapofungua tu sura ya kitabu cha Biblia.)

  • Bofya alama ya Tafsiri Nyingine katika safu ya Habari za Utafiti ili kupata tafsiri mbalimbali za mstari huo.

  • Bofya alama ya Marejeo ya pambizoni katika safu ya Habari za Utafiti ili kupata orodha ya marejeo yote ya pambizoni ya sura hiyo.

Kitufe cha Hazina

Kitufe cha Hazina huanza kwa maelezo mafupi ya sura hiyo yaliyo katika mambo makuu ya kitabu hicho cha Biblia.

Mwisho wa maelezo mafupi, huenda ukaona mambo yafuatayo kwa ajili ya kila mstari wa sura:

  • Habari za Utafiti: Ni habari za utafiti za mstari huo.

    Bofya kiunganishi cha habari za marejeleo kama vile Maneno ya Kamusi au makala za Nyongeza kisanduku cha makala hiyo itokee.

  • Picha na Video: Ni picha au video za mstari huo. Bofya picha au maelezo ya picha kufungua Picha au Video.

  • Maelezo ya chini: Maelezo ya ziada ya maneno au semi zilizotumiwa katika mstari huo.

  • Marejeo ya Pambizoni: Marejeo ya neno au semi fulani zilizotumiwa katika mstari huo wa Biblia. Bofya alama ya kujumlisha (+) kufungua marejeo ya mstari huo wa Biblia, au bofya alama ya kutoa (-) kufunga marejeo hayo.

Katika safu ya Maandiko ya Biblia, bofya namba ya mstari, alama ya maelezo ya chini, au herufi za marejeo ili kufungua habari za utafiti za mstari hususa katika safu ya Habari za Utafiti.

Kitufe cha Tafsiri Nyingine

Kitufe cha Tafsiri Nyingine kinaonyesha jinsi mstari huo ulivyotafsiriwa katika Biblia nyingine. Chagua mstari mwingine katika safu ya Maandiko ya Biblia ili kuona tafsiri mbalimbali za mstari huo.

Kitufe Marejeo ya Pambizoni

Kitufe cha Marejeo ya Pambizoni huonyesha marejeo yote ya sura hiyo, na imegawanyika katika sehemu tatu:

  1. Masimulizi yanayopatana: Huonyesha marejeo ya matukio yanayolingana, yaliyo katika vitabu au sura tofauti.

  2. Manukuu: Huonyesha mistari ya Biblia iliyonukuliwa katika sura hiyo.

  3. Jumla: Yanatia ndani marejeo yaliyo na habari zaidi kuhusu mtu au mahali, kutumiwa kwa maneno fulani, utimizo wa unabii, au ufafanuzi wa kanuni fulani zinazohusiana.

Kila mara, bofya alama ya kujumlisha (+) kufungua vipengele vya marejeo ya pambizoni ya mstari wa Biblia, au bofya alama ya kutoa (-) kufunga vipengele hivyo.

Bofya Visanduku vilivyo mbele ya sehemu hizo tatu ili kutia alama herufi za marejeo katika safu ya Maandiko ya Biblia. Hiyo itakusadia, ikiwa unataka kujua mistari yote ambayo mwandishi wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo alinukuu kutoka Maandiko ya Kiebrania.

 Tazama picha na video za kitabu cha Biblia

Picha na Video ni mfululizo wa picha na video za kila kitabu cha Biblia. Picha na video zimepangwa kulingana na mfuatano wa matukio ya kitabu hicho.

Tumia njia zifuatazo kufungua Picha au Video:

  • Bofya picha iliyo katika safu ya Habari za Utafiti.

  • Katika ukurasa wa Yaliyomo au katika orodha ya vitabu, bofya Picha na Video.

Kipengele cha Picha na Video kina sehemu tatu:

  1. Picha au video. Bofya Kishale cha Kushoto kutazama picha zilizo nyuma au Kishale cha Kulia kutazama picha zilizo mbele.

  2. Maelezo ya picha na orodha ya maandiko mengine yanayohusishwa na picha hiyo katika safu ya Habari za Utafiti.

    Katika vifaa vya mkononi, bofya alama ya Mshale Unaoelekezea Juu ili kusoma maelezo ya picha au Mshale Unaoelekezea Chini ili kuyaficha.

  3. Mpangilio wa picha ndogondogo. Bofya Kishale cha Kushoto kutazama picha zilizo nyuma au Kishale cha Kulia kutazama picha zilizo mbele. Bofya picha hiyo ndogo ili kuitazama.

Ikiwa umefungua picha yenye maelezo ya picha hiyo, bofya kitufe cha Cheza ili kucheza sauti iliyorekodiwa ya maelezo hayo.

Ili kutazama video, tumia alama za kifaa chako kucheza, kusimamisha au kuikuza video.

 Tumia muhtasari wa vitabu vya Biblia, kamusi ya maneno au nyongeza

Kuna njia mbili za kupata sehemu hizo:

  • Bofya herufi ya marejeo katika safu ya Habari za Utafiti.

  • Chagua kitabu kimoja katika ukurasa wa Yaliyomo au kwenye orodha ya vitabu.

Baadhi ya nyongeza zinatumia njia mbili kuweka habari katika mtindo wa picha moja (ya ukurasa fulani kwenye Tafsiri ya Ulimwengu Mpya) au katika mtindo wa habari zilizo na picha.

  • Fungua katika mtindo wa picha moja. Bofya picha ili ifunguke.

  • Fungua katika mtindo wa habari zilizo na picha tofauti. Njia hii inakuruhusu kufungua viunganishi vya andiko na marejeo mengine na kusoma habari zake katika safu ya Habari za Utafiti.