Ona video zinazopatikana

TAREHE 29 MWEZI WA 8, 2017
ANGOLA

Mashahidi Kwenye Mukusanyiko Katika Inchi ya Angola Wanasumbuliwa na Gaze Yenye Sumu

Mashahidi Kwenye Mukusanyiko Katika Inchi ya Angola Wanasumbuliwa na Gaze Yenye Sumu

Asubui ya Siku ya Tano tarehe 25 Mwezi wa 8, 2017, wakati mukusanyiko ulikuwa unafanywa katika Jumba la Mukusanyiko la Viana huko Luanda, Angola, wahuzuriaji 405 walizimia wakati washambuliaji waliwapulizia gaze yenye sumu katika jumba kubwa na katika vyoo ao WC. Jambo la kufurahisha ni kwamba gaze hiyo haikuwa hatari na hakuna mutu mwenye alikufa. Watu wenye walipumua gaze hiyo walipelekwa katika hospitali na wengi wao walitunzwa na kuruhusiwa warudie nyumbani kisha saa kidogo. Uchunguzi unafanywa na wenye mamlaka; wanaume watatu walikamatwa na kupelekwa kwenye biro ya polisi Siku ya Tano muchana.

Ofisi ya tawi ya Luanda imesema kwamba watu hao wote wanajisikia muzuri. Wahuzuriaji kwenye mukusanyiko hawakuogopa sana na walifanya kazi pamoja ili kuwasaidia wale wenye walipumua gaze hiyo. Kwa sababu ya mapendekezo ya polisi, kipindi cha mukusanyiko cha kisha midi cha Siku ya Tano hakikufanywa. Hata hivyo, Siku ya Posho tarehe 26 Mwezi wa 8, na Siku ya Yenga tarehe 27 Mwezi wa 8, mukusanyiko uliendelea bila matatizo. Huzurio lilifikia watu zaidi ya 12 000, na 188 walibatizwa na kuwa Mashahidi wa Yehova.

Watangazaji wa Habari Wanaweza Kuzungumuza na:

David A. Semonian, Biro ya Kutoa Habari, tel. +1-845-524-3000

Angola: Todd Peckham, tel. +244-923-166-760