Ona video zinazopatikana

(Kushoto) Hatua za kutusaidia kujilinda, kutia ndani kusafisha kwenye tunaishi na pia Jumba yetu ya Ufalme; (Katikati) Mu maeneo fulani yenye kupigwa na ile ugonjwa, wahubiri wanaweza kuchagua kufanya aina zingine za mahubiri, kama kuhubiri kupitia telefone; (Kuume) Mu maeneo yenye kupigwa na ile ugonjwa, kulingana na hali, wazee wanaweza kusaidia ndugu wapate mikutano yenye kurekodiwa

TAREHE 3, MWEZI WA 3, 2020
HABARI ZA DUNIA YOTE

Ripoti ya Ugonjwa wa Coronavirus na Namna Tunaweza Kujilinda

Ripoti ya Ugonjwa wa Coronavirus na Namna Tunaweza Kujilinda

Ndugu wa makao makubwa ya Mashahidi wa Yehova wanaendelea kufuatilia kwa uangalifu habari kuhusu ugonjwa wa coronavirus (ao COVID-19). Wanaendelea pia kusikiliza onyo ya wakubwa wa serikali ili kutusaidia tujue namna ya kujilinda. Kupitia unabii wa Biblia, tunajua kama magonjwa ya kuambukiza ni sehemu ya alama ya siku za mwisho. (Luka 21:11) Wakati ugonjwa unaanza kusambaa, ni jambo ya hekima kukamata mipango ya kujilinda na kulinda watu wengine.​—Mezali 22:3.

Wengine wanaweza kupenda kujua hali ya ndugu na dada zetu wa mu maeneo yenye kushambuliwa sana na ile ugonjwa. Ugonjwa wa COVID-19 ulifanya biro za tawi na makutaniko ya Italia, Japani, Korea ya Kusini, na inchi zingine zifanye mabadiliko fulani. Mu hali fulani, biro ya tawi haikuruhusu watu wakuye kutembelea Beteli. Serikali pia hazikuruhusu tena mikutano ya watu wengi. Ile ilifanya biro ya tawi isiruhusu kukuwe mikusanyiko ya muzunguko. Tena, makutaniko ilipaswa kubadilisha namna yao ya kuhubiri na kukusanyika. Hata kama ile magumu ilitokea, ndugu zetu wanaendelea kusoma, kujifunza Biblia, na kutiana moyo.​—Yuda 20, 21.

Mu hali za vile, ndugu zetu waliona kanuni zenye kuonyeshwa hapa chini, kuwa zenye kusaidia. Hii mambo inaweza kukusaidia weye na watu wa familia yako wakati ile ugonjwa inatokea na kusambaa kwenye unaishi.

  • Usiogope. Hata kama ni muzuri kuwa macho wakati magonjwa yenye kuambukiza inatokea na kukamata maamuzi yenye kufaa, tusiache woga itufanye tukamate maamuzi yenye haiko ya hekima.​—Mezali 14:15; Isaya 30:15.

  • Fuata Muongozo wa Wakubwa wa Serikali. Mara mingi wakubwa wa serikali mu hali za hivi wanatiaka sheria za kulinda watu. Ni muzuri kuzijua na kutii muongozo wa wakubwa wa serikali.​—Waroma 13:1.

  • Usafi Ni wa Lazima Sana. Ni jambo ya lazima sana kunawa mikono kwa ukawaida kwa kutumia sabuni na maji ao kupakaa ku mikono dawa fulani yenye kuwa na alkoholi. Tusafishe kwa ukawaida kwenye tunaishi na pia Jumba yetu ya Ufalme. Tena, watu wenye kuhangaikia mambo ya afya wanaonyesha kama kusalimiana kwa mikono inaweza kufanya ile ugonjwa isambae. Kuhusu coronavirus, Shirika ya Afya Ulimwenguni ilitolea watu mashauri ingine.

  • Onyesha Wengine Upendo. Tunajua kama ni jambo ya lazima sana kukusanyika na kuhubiri. Lakini, kama uko mugonjwa, ni muzuri ubakie ku nyumba juu usiambukizie wengine. Ile itaonyesha kama unapenda ndugu na dada na majirani wetu wenye hawako Mashahidi.​—Matayo 22:39.

  • Heshimia Mabadiliko ya Muda Kuhusu Mipango ya Kutaniko. Mu maeneo kwenye kuwa ile ugonjwa, inaweza kuwa muzuri biro ya tawi isiruhusu kwanza kwa wakati fulani mikutano ya kutaniko, mikusanyiko, na matukio ingine ya kiteokrasi. Ni vile imekuwa mu inchi zenye kupigwa kabisa na COVID-19, inchi kama vile Italia, Japani, na Korea ya Kusini. Kulingana na hali, wazee wanaweza kuomba ndugu wafuate mikutano yenye kurekodiwa, yenye wahubiri wanaweza kufuata kwao. Wahubiri wanaweza kuhubiri kupitia telefone, sms, Enternete, ao barua.