Ona video zinazopatikana

TAREHE 4 MWEZI WA 10, 2017
URUSI

Tribinali ya Kusikiliza Tena Inatoa Uamuzi wa Kuendelea Kufunga kwa Muda Dennis Christensen

Tribinali ya Kusikiliza Tena Inatoa Uamuzi wa Kuendelea Kufunga kwa Muda Dennis Christensen

Tarehe 28 Mwezi wa 9, 2017, kisha kusikiliza kwa saa tatu, Tribinali ya Eneo ya Oryol ilikataa ombi la kufunguliwa kwa Dennis Christensen, Shahidi wa Yehova mwenye kuwa mwanainchi wa Denmaki. Ataendelea kufungwa kwa muda mupaka tarehe 23 Mwezi wa 11, 2017.

Wakati mashitaka ya Christensen yalikuwa yanasikilizwa katika Mwezi wa 7, muamuzi wa tribinali aliendeleza bila haki kifungo chake mupaka Mwezi wa 11, pengine ili kusaidia wale wenye walimushitaki wakusanye “ushahidi” wenye kuonyesha kuwa iko na musimamo mukali. Watetezi wa Christensen’ walijaza ombi la kusikilizwa kwenye Tribinali ya Haki za Kibinadamu ya Ulaya, na katika tarehe 4 Mwezi wa 9, 2017, tribinali hiyo ilianza kuchunguza mashitaka hayo kwa kutuma maulizo mbalimbali katika Urusi juu ya kuvunjwa kwa haki za Christensen.

Watu katika dunia yote wanafuata kwa uangalifu mashitaka hayo juu ya Christensen kwa sababu yako kati ya mashitaka ya kwanza tangu wakati wa utawala wa Sovieti yenye Urusi imefunga Shahidi kwa sababu tu ya imani yake.