Ona video zinazopatikana

TAREHE 30 MWEZI WA 8, 2017
VENEZUELA

Mashahidi wa Yehova Katika Venezuela Wanaendelea Kufundisha Watu Biblia Hata Kama Kuko Matatizo ya Feza

Mashahidi wa Yehova Katika Venezuela Wanaendelea Kufundisha Watu Biblia Hata Kama Kuko Matatizo ya Feza

NEW YORK—Vyombo vya kutangaza habari vya kimataifa vimekuwa vikitoa habari juu ya namna hali inaendelea kuharibika katika inchi ya Venezuela kwa sababu ya matatizo ya feza. Halmashauri ya Tawi ya Venezuela inasema kama ndugu na dada zetu wamepatwa pia na matatizo hayo. Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi Yehova linahangaishwa sana kwa sababu ya habari hizo.

Wezi wenye kuwa na silaha wameingia katika Majumba fulani ya Ufalme wakati mikutano ya kila juma inafanywa ili kuiba vyombo mbalimbali vya kielektronike na vitu vingine vya maana. Zaidi ya hilo, katika hali fulani, mikutano inafanywa katika nyumba za ndugu na dada kwa sababu mapigano yenye jeuri inafanya wasiweze kufika kwenye Majumba ya Ufalme. Ndugu na dada wako kati ya watu wengi wenye wamepoteza kazi zao kwa sababu mahali kwenye walikuwa wanatumika kumefungwa. Ndugu fulani wenye walikuwa na biashara yao wamewindwa na watu wabaya wenye jeuri, na kwa hiyo, wamelazimika kuuzisha biashara yao na kukimbilia katika inchi ingine kwa sababu ya usalama wao. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, kwa miaka fulani yenye imepita, kumekuwa ndugu na dada 680 hivi wenye wamechukuliwa kwa nguvu, wezi wenye kuwa na silaha wameingilia Mashahidi zaidi ya 13 146, na 144 wamelalwa kinguvu ao kuwa katika hatari ya kulalwa kinguvu. Jambo la kuhuzunisha sana ni kwamba, ripoti ya tarehe 10 Mwezi wa 8, 2017, inaonyesha kama ndugu na dada 47 wameuawa. Wengine wamekufa kwa sababu hawakuweza kupata matunzo yenye kufaa.

Baraza Lenye Kuongoza linafuata kwa uangalifu namna hali inaendelea, na linatumia michango yenye kutolewa ili kusaidia ndugu na dada wenye wanahitaji vitu vya lazima. Baraza Lenye Kuongoza linazungumuza pamoja na tawi zingine katika dunia yote ili kujua namna ya muzuri ya kutegemeza ndugu na dada katika Venezuela, kwa sababu kutoa michango moja kwa moja inaweza kuwa hatari.

Halmashauri ya Tawi ya Venezuela imefanya halmashauri ya kutoa misaada ya haraka kwenye biro ya tawi yenye kusimamia halmashauri zingine ndogo-ndogo 24 katika inchi yote ili kutimiza mahitaji ya ndugu zetu. Zaidi ya wahubiri 149 000 katika Venezuela hawavumilie tu mateso mbalimbali katika “siku za mwisho,” lakini pia wanaendelea kujikaza kuzungumuza na majirani wao juu ya ujumbe wa Biblia wenye kutuliza. (2 Timotheo 3:1-5; 2 Timotheo 4:2) Luis R. Navas, musemaji wa biro ya tawi ya Venezuela anasema hivi: “Kuliko wakati mwengine wowote, tumekuwa na maendeleo mengi ya kiroho. Watu wenye kuhuzuria mikutano ya kutaniko wameongezeka. Wahubiri wengi wamekuwa mapainia wa kawaida na wakati huohuo wanaendelea kuwa waangalifu sana wakati wako katika kazi ya kuhubiri. Kwa sababu majirani wetu wanajua kama hatujiingize hata kidogo katika mambo ya politike na hatujiingize katika mambo yoyote yenye jeuri yenye kuenea katika inchi, wanakubali ujumbe wa Biblia wenye kutoa tumaini na kitulizo wenye tunawatolea.”

Mashahidi wa Yehova katika Venezuela wataendelea kuhangaikiana na kutuliza majirani wao. Katika dunia yote, ndugu na dada zao wataendelea kuwategemeza na kusali kwa ajili yao.—Waroma 12:12, 13; 2 Wakorintho 1:3, 4.

Watangazaji wa habari wanaweza kuzungumuza na:

David A. Semonian, Biro ya Kutoa Habari, tel. +1-845-524-3000

Venezuela: Luis R. Navas, tel. +58-244-400-5000