Cha Pili cha Samweli 8:1-18

  • Ushindi mbalimbali wa Daudi (1-14)

  • Namna utawala wa Daudi ulipangwa (15-18)

8  Kisha wakati fulani, Daudi alishinda Wafilisti+ na kuwatiisha,+ na akakamata Meteg-ama kutoka katika mikono ya Wafilisti.  Akashinda Wamoabu+ na akawalalisha chini na kuwapima kwa kamba. Alipima kamba mbili za kuuawa, na kamba moja nzima yenye haitauawa.+ Na Wamoabu wakakuwa watumishi wa Daudi na wakaleta ushuru.+  Daudi akamushinda Hadadezeri mwana wa Rehobu mufalme wa Soba+ wakati alikuwa anaenda kurudisha mamlaka yake kwenye Muto Efrati.+  Daudi akakamata kutoka kwake wapanda-farasi elfu moja na mia saba (1 700) na maaskari elfu makumi mbili (20 000) wenye kutembea kwa miguu. Kisha Daudi akakata farasi wote wa magari mishipa ya magoti lakini akaacha mia moja (100) kati yao.+  Wakati Wasiria wa Damasko+ walikuja kumusaidia Mufalme Hadadezeri wa Soba, Daudi alipiga na kuua Wasiria elfu makumi mbili na mbili (22 000).+  Halafu Daudi akaweka kambi za kijeshi katika Siria ya Damasko, na Wasiria wakakuwa watumishi wa Daudi na wakaleta ushuru. Yehova alimupatia Daudi ushindi* kila mahali kwenye alienda.+  Tena, Daudi ­alikamata ngao za muviringo za zahabu kutoka kwa watumishi wa Hadadezeri na akazileta Yerusalemu.+  Kutoka Beta na Berotai, miji ya Hadadezeri, Mufalme Daudi alikamata shaba nyingi sana.  Sasa Mufalme Toi wa Hamati+ akasikia kwamba Daudi alikuwa ameshinda jeshi lote la Hadadezeri.+ 10  Kwa hiyo Toi akamutuma Yoramu mwana wake kwa Mufalme Daudi ili aulize hali yake na kumupongeza kwa sababu alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumushinda (kwa maana Hadadezeri alikuwa amepigana na Toi mara nyingi); na alimuletea vitu vya feza, zahabu, na shaba. 11  Mufalme Daudi akatakasa vitu hivyo kwa ajili ya Yehova, pamoja na ile feza na ile zahabu yenye alikuwa ametakasa kutoka kwa mataifa yote yenye alikuwa ametiisha:+ 12  kutoka Siria na kutoka Moabu,+ kutoka kwa Waamoni, Wafilisti,+ Waamaleki,+ na kutoka katika vitu vyenye vilichukuliwa kwa Hadadezeri+ mwana wa Rehobu mufalme wa Soba. 13  Pia Daudi alijifanyia jina wakati alirudia kisha kupiga na kuua Waedomu elfu kumi na munane (18 000) katika Bonde la Chumvi.+ 14  Akaweka kambi za kijeshi katika Edomu. Aliweka kambi za kijeshi katika Edomu yote, na Waedomu wote wakakuwa watumishi wa Daudi.+ Yehova alimupatia Daudi ushindi* kila mahali kwenye ­alienda.+ 15  Daudi akaendelea kutawala juu ya Israeli yote,+ na Daudi alikuwa anatenda haki na uadilifu*+ kwa ajili ya watu wake wote.+ 16  Yoabu+ mwana wa Seruya alikuwa mukubwa wa jeshi, na Yehoshafati+ mwana wa Ahiludi alikuwa karani. 17  Sadoki+ mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiatari walikuwa makuhani, na Seraya alikuwa mwandishi. 18  Benaya+ mwana wa Yehoyada alisimamia Wakereti na Wapeleti.+ Na wana wa Daudi wakakuwa watumishi wakubwa.*

Maelezo ya Chini

Ao “wokovu.”
Ao “wokovu.”
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “wakakuwa makuhani.”