Amosi 8:1-14

  • Maono ya kitunga cha matunda ya kipindi cha joto (1-3)

  • Wakandamizaji wanalaumiwa (4-14)

    • Njaa ya kiroho (11)

8  Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova alinionyesha mambo haya: Angalia! Kulikuwa kitunga cha matunda ya kipindi cha joto.  Kisha akasema, “Unaona nini, Amosi?” Nikajibu, “Kitunga cha matunda ya kipindi cha joto.” Basi Yehova akaniambia: “Mwisho umefikia watu wangu Israeli. Sitawasamehe tena.+  ‘Siku hiyo nyimbo za hekalu zitageuka kuwa maombolezo,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema. ‘Kutakuwa mizoga mingi yenye kutupwa kila mahali+—kimya!’   Musikie jambo hili, ninyi wenye kukanyanga maskini Na kuharibu wapole wa inchi,+   Wenye kusema, ‘Sikukuu ya mwezi mupya itaisha wakati gani,+ ili tuuzishe nafaka yetu, Na Sabato+ itaisha wakati gani, ili tuweze kuuzisha nafaka? Ili tupunguze vipimo vya efa* Na kuongeza uzito wa shekeli,* Ili kupotosha mizani* zetu za udanganyifu;+   Ili tununue watu wenye kuwa katika uhitaji wa feza Na maskini kwa bei ya viatu mbili,+ Na kuuzisha sehemu yenye haina mafaa yoyote ya nafaka.’   Yehova ameapa kwa Kiburi cha Yakobo,+ ‘Sitasahau hata kidogo matendo yao yote.+   Kwa sababu hiyo inchi* itatetemeka, Na kila mukaaji mwenye kuwa ndani yake ataomboleza.+ Je, inchi yote haitapanda kama vile Muto Nile, Na kupanda na kushuka kama vile Muto Nile wa Misri?’+   ‘Katika siku hiyo,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema, ‘Nitafanya jua lishuke katikati ya muchana, Na nitafanya inchi ikuwe na giza wakati wa muchana.+ 10  Nitageuza sikukuu zenu kuwa maombolezo+ Na nyimbo zenu zote kuwa nyimbo za huzuni.* Nitatia nguo za magunia kwenye viuno vyote na kufanya kila kichwa kikuwe na upara; Nitafanya siku hiyo kuwa kama siku ya kuomboleza kifo cha mwana wa pekee, Na mwishowe siku hiyo itakuwa siku ya uchungu.’ 11  ‘Angalia! Siku zinakuja,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema, ‘Wakati nitatuma njaa katika inchi, Hapana njaa ya mukate ao kiu ya maji, Lakini ya kusikia maneno ya Yehova.+ 12  Wataenda wakiyumba-yumba kutoka bahari mupaka bahari Na kutoka kaskazini mupaka mashariki.* Watatanga-tanga huku na huku wakitafuta neno la Yehova, lakini hawatalipata. 13  Siku hiyo mabikira wenye sura na umbo ya muzuri watazimia Pia vijana wanaume watazimia, kwa sababu ya kiu; 14  Wale wenye kuapa kwa hatia ya Samaria+ na kusema, “Kama vile hakika mungu wenu anaishi , Ee Dani!”+ Na, “Kama vile hakika njia ya Beer-sheba+ inaishi!” Wataanguka, na hawatasimama tena.’”+

Maelezo ya Chini

Ao “kilo.”
Ao “dunia.”
Ao “nyimbo za maombolezo.”
Ao “mahali jua linatokea.”