Kutoka 32:1-35

  • Ibada ya sanamu ya kitoto-dume cha ngombe cha zahabu (1-35)

    • Musa anasikia nyimbo za namna ingine (17, 18)

    • Musa anavunja-vunja mabamba ya sheria (19)

    • Walawi wanabakia washikamanifu kwa Yehova (26-29)

32  Wakati huo, watu wakaona kwamba Musa alikawia kushuka kutoka kwenye mulima.+ Kwa hiyo watu wakakusanyika kumuzunguka Haruni na kumuambia: “Simama, ututengenezee mungu mwenye ataenda mbele yetu,+ kwa sababu hatujue kile kimemufikia huyu Musa, ule mutu mwenye alitutosha katika inchi ya Misri.”  Basi Haruni akawaambia: “Mutoshe mahereni ya masikio+ ya zahabu kwenye masikio ya bibi zenu, ya watoto wenu wanaume, na ya watoto wenu wanamuke na muniletee.”  Kwa hiyo watu wote wakaanza kutosha mahereni ya masikio ya zahabu zenye zilikuwa kwenye masikio yao na kuzileta kwa Haruni.  Kisha akakamata zahabu kutoka kwao, na akatengeneza nayo sanamu* ya kitoto-dume cha ngombe kwa kutumia kifaa cha kuchongea.+ Watu wakaanza kusema: “Huyu ndiye Mungu wako, Ee Israeli, mwenye alikuongoza kutoka katika inchi ya Misri.”+  Wakati Haruni aliona jambo hilo, akajenga mazabahu mbele ya sanamu hiyo. Kisha akasema hivi kwa sauti kubwa: “Kesho kutakuwa sikukuu kwa ajili ya Yehova.”  Kwa hiyo wakaamuka asubui sana siku yenye ilifuata na kuanza kutoa matoleo ya kuteketezwa na zabihu za ushirika. Kisha mambo hayo watu wakakaa ili kula na kunywa. Kisha wakasimama ili kujifurahisha.+  Sasa Yehova akamuambia Musa: “Uende, ushuke, kwa sababu watu wako, wenye uliongoza kutoka katika inchi ya Misri, wamejipotosha.+  Wamegeuka haraka na kuacha njia yenye niliwaamuru wafuate.+ Wamejifanyia sanamu* ya kitoto-dume cha ngombe, na wanaendelea kuiinamia na kuitolea zabihu na kusema, ‘Huyu ndiye Mungu wako, Ee Israeli, mwenye alikuongoza kutoka katika inchi ya Misri.’”  Yehova akaendelea kumuambia Musa: “Nimeona kwamba watu wako kichwa-nguvu.*+ 10  Kwa hiyo sasa niache, niwaharibu kwa kasirani yangu yenye kuwaka, na uache nikufanye wewe kuwa taifa kubwa pa nafasi yao.”+ 11  Kisha Musa akamulilia* Yehova Mungu wake+ na kusema: “Ee Yehova, sababu gani ugeuzie kasirani yako yenye kuwaka juu ya watu wako kisha kuwatosha katika inchi ya Misri kwa nguvu kubwa na kwa mukono wenye nguvu?+ 12  Sababu gani Wamisri waseme, ‘Alikuwa na nia mubaya wakati aliwatosha Misri. Alitaka kuwaua katika milima na kuwaangamiza wasikuwe tena juu ya uso wa dunia’?+ Acha kasirani yako yenye kuwaka na ubadilishe nia* kuhusu uamuzi wako wa kuleta musiba huu juu ya watu wako. 13  Kumbuka watumishi wako Abrahamu, Isaka, na Israeli, wenye uliapia kwa jina lako mwenyewe na kusema, ‘Nitafanya uzao wenu ukuwe mwingi* kama nyota za mbinguni,+ na nitapatia uzao wenu* inchi yote hii yenye niliwaahidi, ili waikamate kuwa uriti wa kudumu.’”+ 14  Kwa hiyo Yehova akabadilisha nia yake* kuhusu musiba wenye alikuwa amesema kwamba ataleta juu ya watu wake.+ 15  Kisha Musa akageuka na kushuka kutoka kwenye mulima akiwa amebeba yale mabamba mbili ya Ushuhuda+ katika mukono wake.+ Mabamba hayo yalikuwa yameandikwa pande zote mbili; yalikuwa yameandikwa upande wa mbele na upande wa nyuma. 16  Mabamba hayo yalitengenezwa na Mungu, na maandishi yenye yalichongwa juu ya mabamba hayo yalikuwa maandishi ya Mungu.+ 17  Wakati Yoshua alianza kusikia makelele ya watu wenye walikuwa wanasema kwa sauti kubwa, akamuambia Musa: “Kuko makelele ya vita katika kambi.” 18  Lakini Musa akasema: “Haiko makelele ya nyimbo za ushindi,*Na haiko makelele ya vilio vya kushindwa;Ninasikia makelele ya nyimbo za namna ingine.” 19  Wakati tu Musa alifika karibu na kambi na kuona ile sanamu ya kitoto-dume cha ngombe+ na dansi, kasirani yake ikaanza kuwaka, na akatupa chini yale mabamba mbili yenye yalikuwa katika mikono yake na akayavunja-vunja chini ya mulima.+ 20  Akakamata ile sanamu ya kitoto-dume cha ngombe yenye walikuwa wametengeneza na akaiteketeza kwa moto na kuiponda-ponda na kuifanya kuwa ungaunga;+ kisha akasambaza ungaunga huo juu ya maji na akalazimisha Waisraeli kunywa maji hayo.+ 21  Na Musa akamuambia Haruni: “Watu hawa walikufanya nini hivi kwamba umeleta zambi kubwa juu yao?” 22  Haruni akajibu: “Usikasirike, bwana wangu. Unajua muzuri kwamba watu hawa wako na muelekeo wa kutenda maovu.+ 23  Kwa hiyo waliniambia, ‘Ututengenezee mungu mwenye ataenda mbele yetu, kwa sababu hatujue kile kimemufikia huyu Musa, ule mutu mwenye alitutosha katika inchi ya Misri.’+ 24  Kwa hiyo niliwaambia, ‘Kila mutu mwenye iko* na zahabu aitoshe na kunipatia.’ Kisha nikaitupa ndani ya moto na hii sanamu ya kitoto-dume cha ngombe ikatokea.” 25  Musa akaona kwamba watu walikosa kujizuia, kwa sababu Haruni alikuwa amewaacha wakose kujizuia, na hivyo wakajizaraulisha mbele ya wapinzani wao. 26  Kisha Musa akasimama katika mulango mukubwa wa kambi na kusema: “Ni nani iko* upande wa Yehova? Akuje hapa kwenye niko!”+ Na Walawi wote wakakusanyika kumuzunguka. 27  Halafu Musa akawaambia: “Yehova Mungu wa Israeli amesema, ‘Kila mumoja wenu ajifunge upanga wake na kupita katika kambi yote, kutoka mulango mukubwa mupaka mulango mukubwa, amuue ndugu yake, jirani yake, na rafiki yake.’”+ 28  Walawi wakafanya kama vile Musa alisema. Kwa hiyo watu karibu elfu tatu (3 000) wakauawa siku hiyo. 29  Kisha Musa akasema: “Mujitakase leo kwa ajili ya Yehova, kwa sababu kila mumoja wenu amemushambulia mwana wake mwenyewe na ndugu yake mwenyewe;+ leo atawapatia baraka.”+ 30  Siku yenye ilifuata, Musa akaambia watu: “Mulitenda zambi kubwa sana, na sasa nitapanda kuenda kwa Yehova ili nione kama ninaweza kufunika zambi yenu.”+ 31  Kwa hiyo Musa akarudia kwa Yehova na kusema: “Watu hawa wametenda zambi kubwa sana! Walijitengenezea mungu wa zahabu!+ 32  Lakini sasa ukipenda, samehe zambi yao;+ kama haiko vile, tafazali, unifute katika kitabu chako chenye umeandika.”+ 33  Hata hivyo, Yehova akamuambia Musa: “Kila mutu mwenye amenitendea zambi, nitamufuta katika kitabu changu. 34  Uende sasa, uongoze watu hao mupaka mahali kwenye nimekuambia. Angalia! Malaika wangu ataenda mbele yako,+ na siku hiyo yenye nitaomba hesabu itolewe, nitaleta azabu juu yao kwa sababu ya zambi yao.” 35  Kisha Yehova akaanza kuletea watu pigo kwa sababu walikuwa wametengeneza sanamu ya kitoto-dume cha ngombe, yenye Haruni alikuwa ametengeneza.

Maelezo ya Chini

Ao “sanamu ya kuyeyushwa.”
Ao “sanamu ya kuyeyushwa.”
Ao “ni wenye shingo ngumu.”
Tnn., “akatuliza uso wa.”
Ao “usikitike.”
Tnn., “mbegu yenu ikuwe nyingi.”
Tnn., “mbegu yenu.”
Ao “akasikitika.”
Ao “tendo lenye nguvu.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”