Ufunuo kwa Yohana 18:1-24

  • Kuanguka kwa “Babiloni Mukubwa” (1-8)

    • “Mutoke kwake, watu wangu” (4)

  • Kuomboleza juu ya kuanguka kwa Babiloni (9-19)

  • Kufurahi mbinguni juu ya kuanguka kwa Babiloni (20)

  • Babiloni atatupwa katika bahari kama jiwe (21-24)

18  Kisha mambo hayo nikaona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka makubwa, na dunia ikaangaziwa kwa utukufu wake.  Na akasema kwa sauti kubwa yenye nguvu: “Ameanguka! Babiloni Mukubwa ameanguka,+ na amekuwa makao ya pepo wachafu na mahali pa kujificha pa kila roho muchafu* na kila ndege muchafu mwenye anachukiwa!+  Kwa maana, kwa sababu ya divai ya tamaa kubwa* ya uasherati* wake, mataifa yote yamenaswa,+ na wafalme wa dunia walifanya uasherati naye,+ na wafanyabiashara* wa dunia walikuwa matajiri kutokana na nguvu za maisha yake ya raha ya bila haya.”  Na nikasikia sauti ingine kutoka mbinguni ikisema: “Mutoke kwake, watu wangu,+ kama hamutaki kushiriki pamoja naye katika zambi zake, na kama hamutaki kupokea sehemu ya mapigo yake.+  Kwa maana zambi zake zimekusanyika pamoja mupaka mbinguni,+ na Mungu amekumbuka matendo yake ya kukosa haki.*+  Mumulipe kama vile alitendea wengine,+ ndiyo, mumulipe mara mbili juu ya mambo yenye alitenda;+ katika kikombe+ chenye alichanganya, mumufanyie muchanganyiko mara mbili.+  Kwa kadiri alijitukuza na kuishi maisha ya raha yenye haina haya, kwa kadiri hiyo mumupatie mateso na maombolezo. Kwa maana anaendelea kusema katika moyo wake: ‘Ninakaa nikiwa malkia, mimi siko mujane, na sitaona maombolezo hata kidogo.’+  Hiyo ndiyo sababu mapigo yake yatakuja katika siku moja, kifo na kuomboleza na njaa, naye atateketezwa kabisa kwa moto,+ kwa sababu Yehova* Mungu, mwenye alimuhukumu, ni mwenye nguvu.+  “Na wafalme wa dunia wenye walifanya uasherati* naye na kuishi naye maisha ya raha ya bila haya watalia na kujipiga-piga kwa huzuni juu yake wakati wataona moshi wenye kutokana na kuteketea kwake. 10  Watasimama mbali kwa sababu ya kuogopa kuteseka kwake, na watasema: ‘Ole, ole, wewe muji mukubwa,+ Babiloni wewe muji wenye nguvu, kwa sababu katika saa moja hukumu yako imefika!’ 11  “Pia, wafanyabiashara wa dunia wanalia na kuomboleza juu yake, kwa sababu hakuna mutu yeyote wa kununua tena biashara yao yenye kujaa, 12  biashara yenye kujaa zahabu, feza, majiwe yenye samani, lulu, nguo ya kitani kizuri, nguo ya rangi ya zambarau, hariri, na nguo ya rangi nyekundu yenye kungaa; na kila kitu chenye kutengenezwa kwa miti yenye harufu ya muzuri; na kila aina ya kitu chenye kutengenezwa kwa pembe za tembo, na kwa mbao za samani, shaba, chuma, na marumaru; 13  pia mudalasini, manukato ya Kihindi, uvumba, mafuta yenye marashi, ubani, divai, mafuta ya zeituni, unga muzuri, ngano, ngombe, kondoo, farasi, magari, watumwa, na uzima wa wanadamu.* 14  Ndiyo, tunda la muzuri lenye ulitamani* limekuacha, na vyakula vyote vitamu na vitu vyenye kupendeza vimepotea kutoka kwako, na havitapatikana tena hata kidogo. 15  “Wafanyabiashara wenye waliuzisha vitu hivyo, wenye walipata utajiri kutokana naye, watasimama mbali kwa sababu ya kuogopa kuteseka kwake na watalia na kuomboleza, 16  wakisema: ‘Ole, ole, ule muji mukubwa, wenye kuvaa nguo ya kitani kizuri, zambarau, na nguo nyekundu yenye kungaa na wenye kupambwa sana kwa mapambo ya zahabu, majiwe yenye samani, na lulu,+ 17  kwa sababu katika saa moja mali nyingi vile zimehari­biwa!’ “Na kila kapiteni wa mashua* na kila mutu mwenye anasafiri katika bahari na watumishi wa mashua na wale wote wenye wanaishi kupitia bahari walisimama mbali 18  na wakalia kwa sauti kubwa wakati uleule wakiangalia moshi wenye kutokana na kuteketezwa kwake: ‘Ni muji gani wenye kuwa kama ule muji mukubwa?’ 19  Wakatupa mavumbi juu ya vichwa vyao na wakapandisha sauti, wakilia na kuomboleza, na wakasema: ‘Ole, ole, ule muji mukubwa, wenye wale wote wenye walikuwa na mashua* katika bahari walikuwa matajiri kutokana na utajiri wake, kwa sababu katika saa moja ameharibiwa!’+ 20  “Mufurahi juu yake, ninyi mbingu,+ pia ninyi watakatifu+ na mitume na manabii, kwa sababu Mungu ametangaza hukumu juu yake kwa ajili yenu!”+ 21  Na malaika mwenye nguvu akainua jiwe lenye lilikuwa kama jiwe kubwa la kusagia na akalitupa katika bahari, na kusema: “Ni vile Babiloni ule muji mukubwa utatupwa kwa nguvu sana, na hautapatikana tena hata kidogo.+ 22  Na sauti ya waimbaji wenye wanafuatanisha sauti zao kwa kinubi, ya wapiga-muziki, ya wapiga-filimbi, na ya wapiga-tarumbeta haitasikiwa tena ndani yako hata kidogo. Na hakuna fundi mwenye anafanya kazi yoyote mwenye atapatikana tena ndani yako, na hakuna sauti ya jiwe la kusagia yenye itasikiwa tena ndani yako. 23  Hakuna mwangaza wa taa wenye utaangaza tena ndani yako, na hakuna sauti ya bwana-arusi na ya bibi-arusi yenye itasikiwa tena ndani yako; kwa maana wafanyabiashara wako walikuwa watu wenye vyeo vya juu wa dunia, na kupitia mazoea yako ya kupashana habari na pepo wachafu+ mataifa yote yalipotoshwa. 24  Ndiyo, ndani yake ilipatikana damu ya manabii na ya watakatifu+ na ya wale wote wenye wameuawa katika dunia.”+

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “pumuzi chafu; neno chafu lenye liliongozwa na roho.”
Ao “kasirani.”
Kigiriki por·neiʹa. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “wafanyabiashara wenye kusafiri.”
Ao “matendo yake ya uovu.”
Ao “nafsi za wanadamu.”
Ao “lenye nafsi yako ilitamani.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”