Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Kuko Siku Magumu Yote Itaisha

Kuko Siku Magumu Yote Itaisha

Ni mwepesi magumu kutuvunja moyo, zaidi sana kama inaendelea. Daudi alijua kama magumu yenye alikuwa nayo juu ya Mufalme Sauli ingeisha, na alijua kama angefikia kuwa mufalme sawa vile Yehova aliahidi. (1Sa 16:13) Imani ya Daudi ilimusaidia angojee Yehova kwa uvumilivu ili amalize magumu yake.

Wakati tuko mu magumu, tunaweza kutumikisha werevu, ujuzi, ao uwezo wetu wa kufikiri juu ya kubadilisha hali yetu. (1Sa 21:12-14; Mez 1:4) Lakini, hata kisha kufanya yote yenye tunaweza na yenye kupatana na kanuzi za Biblia, kuko magumu yenye inaweza kuendelea tu. Mu njia za vile, tunapaswa kuwa wavumilivu na kumungojea Yehova. Hivi karibuni, atamaliza magumu na mateso yetu yote, na “atapanguza kila chozi” mu macho yetu. (Ufu 21:4) Ikuwe Yehova anafanya jambo fulani ili kututuliza, ao tunatulizwa kupitia nja ingine, tunapaswa kuwa hakika na hii jambo: Kuko siku magumu yote itaisha. Kujua vile inaweza kutufariji.

MUANGALIE VIDEO WATU WENYE KUUNGANA MU DUNIA YENYE KUGAWANYIKA, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Ni magumu gani yenye Wakristo fulani walipata mu sehemu ya kusini ya Amerika?

  • Namna gani walionyesha uvumilivu na upendo?

  • Namna gani waliendelea ‘kuhakikisha mambo ya maana zaidi’?​—Flp 1:10