Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Onyesha Upendo Katika Familia

Onyesha Upendo Katika Familia

Upendo uko sawa vile colle yenye inaunganisha familia. Bila upendo, ni nguvu kwa watu wa familia kuishi kwa umoja na kwa upatano. Namna gani bibi, bwana, na wazazi wanaweza kuonyesha upendo mu familia?

Bwana mwenye upendo anafikiriaka mambo yenye bibi yake iko nayo lazima, anafikiriaka vile iko anajisikia na anasikilizaka mawazo yake. (Efe 5:28, 29) Anapatia familia yake mahitaji ya kiroho na ya kimwili. Ile inatia ndani kufanya Ibada ya Familia kwa ukawaida. (1Ti 5:8) Bibi mwenye upendo anajitiishaka kwa bwana yake na “kumuheshimia sana.” (Efe 5:22, 33; 1Pe 3:1-6) Bibi na bwana wanapaswa kusameheana kwa kupenda. (Efe 4:32) Wazazi wenye upendo wanapendezwa na kila mutoto wao na wanawafundisha ili wamupende Yehova. (Kum 6:6, 7; Efe 6:4) Ni magumu gani yenye watoto wenu wanapambana nayo ku masomo? Wakati vijana wenzao wanawakaza kufanya mambo fulani, wanafanyaka nini? Kama watu mu familia wanapendana sana, watajisikia kuwa salama na wenye kulindwa.

MUANGALIE VIDEO ONYESHA UPENDO WA KWELI KATIKA FAMILIA YAKO, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Namna gani bwana mwenye upendo anaonyesha kama anahangaikia na kupenda bibi yake?

  • Bibi mwenye upendo anafanya nini ili kuonyesha kama anaheshimia bwana yake?

  • Wazazi wenye upendo wanafanya nini ili kukazia katika watoto wao Neno la Mungu?