Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuacha Kuongoza Mafunzo Yenye Haifanye Maendeleo

Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuacha Kuongoza Mafunzo Yenye Haifanye Maendeleo

SABABU GANI NI LAZIMA: Watu wanapaswa kuitia jina la Yehova juu waokolewe. (Ro 10:13, 14) Hata kama mutu anaitika kujifunza Biblia, ile haimaanishe kama anapenda kuishi kulingana na kanuni za Yehova. Tunapaswa kutumia muzuri wakati yetu mu mahubiri kwa kusaidia wale wenye wanapenda kabisa kufanya mabadiliko juu wamufurahishe Yehova. Kama mwanafunzi wa Biblia hafanye kabisa maendeleo kisha kujifunza naye mu wakati fulani, ni muzuri tuache kujifunza naye na tutumie wakati yetu juu ya kusaidia wale wenye Yehova iko anavuta kwake na mu tengenezo lake. (Yoh 6:44) Lakini, kisha wakati fulani, ikionekana kama mwanafunzi anafanya mabadiliko na anaonyesha kama ‘iko na muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele,’ tutaanza tena kujifunza naye.​—Mdo 13:48.

NAMNA YA KUFANYA:

  • Upongeze mwanafunzi juu ya nia yake ya kupenda kupata ujuzi wa kweli.​—1Ti 2:4

  • Umuonyeshe kama ni jambo ya lazima sana atumikishe mambo yenye amejifunza.​—Lu 6:46-49

  • Kwa upole, zungumuza naye kuhusu mufano wa Yesu wa mupandaji, na umuombe ajiulize ni nini inamuzuia kufanya maendeleo.​—Mt 13:18-23

  • Bila kumukwaza, umuonyeshe juu ya nini hautaendelea tena kujifunza naye

  • Umuonyeshe kama utakuwa unapita kumuona wakati fulani juu ya kumutia moyo na kwamba inawezekana uanze tena kujifunza naye mu siku zenye kuja kama anafanya maendeleo

MUANGALIE VIDEO, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Mu mazunguzo yenye tumetoka kuona, nini njo inaonyesha kama mwanafunzi hakukuwa anafanya maendeleo ya kiroho?

  • Muhubiri alifanya nini juu asaidie mwanafunzi aelewe kama ni jambo ya lazima sana afanye mabadiliko?

  • Muhubiri alisaidia namna gani mwanafunzi aelewe kama funzo inaweza kuanza tena akifanya mabadiliko?