Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Unaona Sifa za Mungu Zenye Hazionekane?

Unaona Sifa za Mungu Zenye Hazionekane?

Wakati unaona maua ya muzuri sana, mbingu yenye kujaa nyota, ao poromoko ya maji yenye kuvuma, je, unatambua kama kuko Muumbaji mwenye alifanya ile yote? Uumbaji wenye kutuzunguka unaonyesha waziwazi sifa za Yehova zenye hazionekane. (Ro 1:20) Kama tunafikiri kuhusu vitu vyenye tunaona na macho yetu, tutatambua kama Mungu iko na nguvu, upendo, hekima, haki, na ni mukarimu.​—Zb 104:24.

Ni vitu gani vyenye Yehova aliumba vyenye unajioneaka kila siku? Hata kama unaishi mu muji mukubwa, pengine unaonaka ndege ao miti. Kuchunguza sana uumbaji wa Yehova kunaweza kutusaidia kupunguza mahangaiko, kukaza akili yetu juu ya mambo ya maana zaidi, na kunaweza kutusaidia tukuwe hakika kabisa kama Yehova ataendelea kutuhangaikia milele. (Mt 6:25-32) Kama uko na watoto, uwasaidie watambue sifa za ajabu za Yehova. Kadiri tutaendelea kufurahia uumbaji wa Yehova wenye kutuzunguka, tutamukaribia zaidi Muumbaji wetu.​—Zb 8:3, 4.

MUANGALIE VIDEO UUMBAJI UNAFUNUA UTUKUFU WA MUNGU​—MWANGAZA NA RANGI, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Rangi mbalimbali zinatokaka wapi?

  • Juu ya nini rangi fulani zinabadilikaka kulingana na kwenye mutu iko anaziangalilia?

  • Juu ya nini tunaonaka rangi mbalimbali mu anga?

  • Ni rangi gani za kupendeza sana zenye umekwisha kuona karibu na weye?

  • Juu ya nini tunapaswa kuwa na zoezi ya kuchunguza sana vitu vyenye Yehova aliumba?

Mwangaza na rangi vinatufundisha nini juu ya Yehova?