Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tarehe 15-21/1

YOBU 36-37

Tarehe 15-21/1

Wimbo 147 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU

1. Juu ya Nini Unaweza Kuamini Kama Tutaishi Milele?

(Dak. 10)

Yehova mwenyewe anaishi milele (Yob 36:26; w15 1/10 uku. 13 fu. 1-2)

Yehova iko na hekima na uwezo wa kufanya uzima uendelee (Yob 36:27, 28; w20.05 uku. 22 fu. 6)

Yehova anatufundisha namna ya kupata uzima wa milele (Yob 36:4, 22; Yoh 17:3)


Kuamini kabisa ahadi ya Mungu ya uzima wa milele kunatupatia nguvu ya kupiganisha magumu ya maisha.—Ebr 6:19; w22.10 uku. 28 fu. 16.

2. Mali ya Kiroho

(Dak. 10)

  • Yob 37:20—Namna gani watu walikuwaka napashana habari zamani mu inchi zenye kuzungumuziwa mu Biblia? (it-1-F uku. 503)

  • Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?

3. Usomaji wa Biblia

TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI

4. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YA MAHALI PA WATU WENGI. (lmd somo ya 3 nukta ya 3)

5. Kuendelesha Mazungumuzo

(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. (lmd somo ya 2 nukta ya 5)

6. Kufasiria Mambo Yenye Unaamini

(Dak. 5) Hotuba. ijwfq 57 fu. 5-15—Kichwa: Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Waliteswa Wakati wa Maangamizi Makubwa ya Wanazi? (th somo ya 18)

MAISHA YA MUKRISTO

Wimbo 49

7. Ujitayarishe kwa Ajili ya Matunzo Yenye Inaomba Upasuaji

(Dak. 15) Mazungumuzo. Itolewe na muzee.

Tengenezo ya Yehova imetutolea vyombo vyenye vinatusaidia tutii sheria ya Mungu juu ya damu. (Mdo 15:28, 29) Unavitumikishaka muzuri?

Karte Pas de sang (DPA) na Carte d’identité (ic): Mu ile madokima, mugonjwa anaandikaka mawazo yake juu ya matunzo yenye inaomba kutumia damu. Muhubiri mwenye kubatizwa anaweza kuomba karte DPA kwa mutumishi wa vichapo, na anaweza kuombea mutoto wake mwenye hayakomala carte d’identité. Tunapaswa kutembea na ile makarte kila fasi na kila wakati. Kama unapenda kuijaza ao kutia habari za sasa, usikawie.

Habari Kwa Ajili ya Mama Wenye Kuwa na Mimba (S-401) na Informations pour les patients devant subir une chirurgie ou une chimiothérapie (S-407): Hii madokima inatusaidia kupunguza hatari na kuepuka hali ya nguvu yenye itaomba kutiwa damu. Kama uko na mimba, kama unataka kufanyiwa upasuaji ao kama unataka kutunziwa kansere, uombe wazee wa kutaniko yenu dokima yenye inapatana na hali yako.

Halmashauri ya Uhusiano na Hopitali (CLH): Ndugu wa CLH ni wazee wenye wamezoezwa juu ya kutolea wanganga na wahubiri habari zenye zinahusu matumizi ya damu. Wanaweza kuongea na munganga wako kuhusu ufundi mbalimbali yenye inaweza kusaidia utunziwe bila kutiwa damu. Kama ni lazima, wanaweza kukusaidia kupata munganga mwenye iko tayari kukubali mawazo yako. Wale wazee wako tayari kusaidia kila siku na saa yoyote. Uite ndugu wa CLH bila kuchelewa mu hali yoyote yenye inaomba ubakie mu hopitali, ufanyiwe upasuaji, ao upate matunzo ya magonjwa ya nguvu sawa vile kansere. Ufanye vile hata kama pengine haitaomba kutiwa damu. Inahusu pia mama wenye wako na mimba. Kama uko na lazima ya kusaidiwa, uombe muzee fulani akusaidie kupata ndugu wa CLH.

Muangalie VIDEO Halmashauri ya Uhusiano na Hopitali —Wanasaidiaka Namna Gani? Kisha uulize wasikilizaji:

Namna gani CLH inaweza kukusaidia kama uko mu hali yenye inaomba upasuaji?

8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko

Maneno ya Kumalizia (Dak. 3) | Wimbo 67 na Sala