Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tarehe 19-25/2

ZABURI 8-10

Tarehe 19-25/2

Wimbo 2 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU

1. “Nitakusifu, Ee Yehova”!

(Dak. 10)

Yehova ni mwema sana kwetu (Zb 8:3-6; w21.08 uku. 3 fu. 6)

Tunamusifu Yehova kwa furaha wakati tunaambia wengine kuhusu kazi zake za ajabu (Zb 9:1; w20.05 uku. 23 fu. 10)

Tunamusifu pia wakati tunamuimbia kwa moyo wote (Zb 9:2; w22.04 uku. 7 fu. 13)

UJIULIZE, ‘Naweza kumusifu Yehova mu njia gani zingine?’

2. Mali ya Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 8:3—Muandikaji wa hii zaburi alimaanisha nini wakati alizungumuzia vidole vya Mungu? (it-1-F uku. 663)

  • Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?

3. Usomaji wa Biblia

TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI

4. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwenye-nyumba anakuambia kama hamuamini Mungu. (lmd somo ya 5 nukta ya 4)

5. Kuendelesha Mazungumuzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Mu mazungumuzo yenye ilitangulia, mwenye-nyumba alikuambia kama hamuamini Mungu lakini anaweza kuzungumuza na weye juu ya mambo yenye inahakikisha kama Muumbaji anakuwaka. (th somo ya 7)

6. Hotuba

(Dak. 5) w21.06 uku. 6-7 fu. 15-18—Kichwa: Saidia Mwanafunzi Wako wa Biblia Amusifu Yehova. (th somo ya 10)

MAISHA YA MUKRISTO

Wimbo 10

7. Namna ya Kufanya Mahubiri ya Wakati Wowote mu Njia ya Kawaida

(Dak. 10) Mazungumuzo.

Njia moya ya kumusifu Yehova zaidi ni kuhubiria watu wenye tunakutanaka nao kila siku. (Zb 35:28) Ku mwanzo, tunaweza kuogopa kuhubiri wakati wowote. Lakini, kama tunajifunza kuanzisha na kuendelesha mazungumuzo, tunaweza kupata matokeo ya muzuri na kufurahia hii aina ya mahubiri!

Muangalie VIDEO Ukuwe Tayari Kutangaza “Habari Njema ya Amani”—Tafuta Nafasi za Kuhubiri. Kisha uulize:

Mu hii video umejifunza mambo gani yenye inaweza kukusaidia upate matokeo ya muzuri mu mahubiri ya wakati wowote?

Hapa chini kuko mawazo kidogo yenye inaweza kukusaidia ujue namna ya kuanza:

  •   Wakati unatoka kwako, ukuwe tayari kuanzisha mazungumuzo kila mara ikiwa nafasi inajitokeza. Sali juu ya ile, na umuombe Yehova akuongoze juu upate watu wenye watapendezwa

  •   Uchangamukie watu na upendezwe kabisa nao. Ujikaze kujua jambo fulani juu ya mutu, yenye inaweza kukusaidia ujue mafundisho ya Biblia yenye itamufurahisha

  •   Mupatiane namba ya telefone, kama inawezekana

  •   Usisikie mubaya kama mazungumuzo yenu inaisha bila weye kumuambia jambo fulani ya mu Biblia

  •   Waza juu ya ule mutu kisha mazungumuzo yenu. Juu ya kuonyesha kama uko namuhangaikia, ukuwe namutumia hata lien ya andiko ya Biblia ao ya habari fulani yenye kuwa ku jw.org

Pima kufanya hivi: Kama mutu anakuuliza, ‘Wikende yako ilipita je?,’ umuambie jambo fulani yenye ulijifunza ku mukutano ao jambo fulani yenye ulifanya mu mahubiri.

8. Mahitaji ya Kutaniko

(Dak. 5)

9. Funzo ya Biblia ya Kutaniko

Maneno ya Kumalizia (Dak. 3) | Wimbo 65 na Sala