Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tarehe 8-14/1

YOBU 34-35

Tarehe 8-14/1

Wimbo 30 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU

1. Wakati Mambo ya Mubaya Inafikia Watu Wazuri

(Dak. 10)

Ukumbuke kama ukosefu wa haki hautokake kwa Yehova hata kidogo (Yob 34:10; wp19.1 uku. 8 fu. 2)

Waovu wanaweza kuonekana sawa vile hawatapata azabu; lakini hawawezi kujificha mbele ya Yehova (Yob 34:21-26; w17.04 uku. 10 fu. 5)

Njia ya muzuri ya kusaidia watu wenye wanatendewa bila haki ni kuwafundisha juu ya Yehova (Yob 35:9, 10; Mt 28:19, 20; w21.05 uku. 6-7 fu. 19-20)

2. Mali ya Kiroho

(Dak. 10)

  • Yob 35:7—Elihu alipenda kusema nini wakati aliuliza Yobu: “[Mungu] anapokea nini kutoka kwako”? (w17.04 uku. 29 fu. 3)

  • Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?

3. Usomaji wa Biblia

TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI

4. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Anzisha funzo ya Biblia. (lmd somo ya 10 nukta ya 3)

5. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Uonyeshe mutu mwenye iko na watoto wenye wangali wadogo namna ya kupata habari zenye zinaweza kusaidia wazazi ku jw.org. (lmd somo ya 1 nukta 4)

6. Kufanya Wanafunzi

MAISHA YA MUKRISTO

Wimbo 58

7. Unapendaka ‘Kuhubiri Neno’ Wakati Wowote?

(Dak. 15) Mazungumuzo.

Paulo alimuambia Timoteo: “Hubiri neno; fanya vile kwa bidii.” (2Ti 4:2) Neno ya Kigiriki yenye inatafsiriwa “fanya vile kwa bidii” ilitumiwa wakati fulani juu ya kuzungumuzia askari ao mulinzi mwenye alikuwa kila mara tayari kutenda. Ile maneno inaeleza muzuri nia yetu ya kuwa kila mara tayari kupata nafasi ya kugeuza mazungumuzo ya kawaida kuwa mahubiri.

Kumupenda Yehova na kuwa wenye shukrani juu ya mambo yote yenye anatufanyia njo kunatuchochea tuambie wengine juu ya sifa zake za muzuri.

Musome Zaburi 71:8. Kisha uulize wasikilizaji:

Ni mambo gani ya muzuri kuhusu Yehova yenye unapendaka kuambia wengine?

Kupenda watu ni jambo ingine yenye inatuchocheaka tuhubiri wakati wowote.

Muangalie VIDEO Namna Mamia ya Watu Walipata Kweli. Kisha uulize:

  •   Namna gani mahubiri ya wakati wowote ilisaidia mamia ya wahubiri wapate mafunzo ya Biblia?

  •   Namna gani wale wenye walikuwa mu madini ingine walipata faida wakati walijifunza kweli?

  • Namna gani kupenda watu kunatuchocheaka tuhubiri wakati wowote?

  • Juu ya nini unawaza kama kuhubiri wakati wowote ni njia ya muzuri ya kusaidia watu wafikie kumujua Yehova?

8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko

Maneno ya Kumalizia (Dak. 3) | Wimbo 138 na Sala