MAISHA YA MUKRISTO
Vijana—Musikawie Kuingia Kupitia ‘Mulango Mukubwa.’
Tunaweza kufikiri kama tutaendelea kuwa vijana na kama ‘siku zenye musiba’ zenye zinatokea wakati wa uzee katika ulimwengu huu wa Shetani hazitatupata. (Mhu 12:1) Kama uko kijana, hauone kama huu ndio wakati wa kujiwekea miradi ya kiroho, kama vile kufanya utumishi wa wakati wote?
‘Tukio lisilotazamiwa linatupata’ sisi wote, na hata vijana. (Mhu 9:11) ‘Hamujui uzima wenu utakuwa namna gani kesho.’ (Yak 4:14) Kwa hiyo, musikawie kujiwekea miradi ya kiroho. Muingie kupitia ‘mulango mukubwa unaoongoza kwenye utendaji’ wakati ungali wenye kufunguliwa kwenu. (1Kor 16:9) Mutapata furaha nyingi sana.
Miradi fulani ya kiroho yenye munaweza kujiwekea:
-
Kuhubiri katika luga ingine
-
Kuwa painia
-
Kusoma masomo mbalimbali ya kiteokrasi
-
Kujitolea katika kazi ya ujenzi
-
Kutumikia kwenye beteli
-
Kuwa mwangalizi wa muzunguko