Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Yehova Anajua Mambo Yenye Tuko Nayo Lazima

Yehova Anajua Mambo Yenye Tuko Nayo Lazima

Mutumwa muaminifu na mwenye busara anatupatia chakula “kwa wakati wenye kufaa.” Ile inaonyesha kama Yehova mwenye kuongoza ule mutumwa anajua mambo ya kiroho yenye tuko nayo lazima. (Mt 24:45) Mikusanyiko yetu ya eneo na mikutano yenye tunafanya katikati ya juma ni kati ya mambo yenye kuhakikisha vile.

MUANGALIE VIDEO RIPOTI YA 2017 YA HALMASHAURI YA UFUNDISHAJI, NA KISHA MUJIBIE MAULIZO YENYE KUFUATA:

  • Kwenye mikusanyiko yetu ya eneo tunafurahia mafundisho yenye tunapata kwa wakati wenye kufaa, nani njo anapaswa kupewa sifa, na juu ya nini?

  • Kazi ya kutayarisha mukusanyiko wa eneo inaanzaka wakati gani?

  • Habari za kujifunza ku mikusanyiko ya eneo zinachaguliwaka namna gani?

  • Kutayarisha mikusanyiko ya eneo kunatia ndani kazi gani?

  • Namna gani njia za kufundisha za ku masomo ya Gileadi zinatumiwa ili kuandika habari zenye tunajifunzaka ku mukutano ya katikati ya juma?

  • Namna gani idara mbalimbali zinatumika pamoja ili kutayarisha buku la mukutano?

Unajisikia namna gani juu ya mambo ya kiroho yenye Yehova anatupatia?