Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tarehe 18-24/11

ZABURI 107-108

Tarehe 18-24/11

Wimbo 7 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU

1. “Mumushukuru Yehova, kwa Maana Yeye Ni Mwema”

(Dak. 10)

Vile tu Yehova aliokoa Baisraeli kutoka Babiloni, ni vile pia alituokoa kutokana na ulimwengu wa Shetani (Zb 107:1, 2; Kol 1:13, 14)

Tunaonyesha kama tunamushukuru Yehova kwa kumusifu mu kutaniko (Zb 107:31, 32; w07-SW 15/4 uku. 20 fu. 2)

Kufikiria mambo yote yenye Yehova alishatufanyia kutatufanya tumushukuru tena zaidi (Zb 107:43; w15 15/1 uku. 9 fu. 4)

2. Mali ya Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 108:9—Inawezekana ni juu ya nini Moabu inalinganishwa na “beseni [ya Mungu] ya kunawia”? (it-2 uku. 303 fu. 5)

  • Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?

3. Usomaji wa Biblia

TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI

4. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. (lmd somo ya 1 nukta ya 4)

5. Kuendelesha Mazungumuzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Ambia musikilizaji kuhusu mupango wa funzo ya Biblia, na umupatie karte ya funzo ya Biblia. (lmd somo ya 9 nukta ya 3)

6. Hotuba

(Dak. 5) ijwyp 90—Kichwa: Namna Gani Ninaweza Kuepuka Mawazo ya Mubaya? (th somo ya 14)

MAISHA YA MUKRISTO

Wimbo 46

7. Tunaimbaka juu ya Kumushukuru Yehova

(Dak. 15) Mazungumuzo.

Kisha Yehova kubaokoa kutokana na jeshi kubwa ya Bamisri mu Bahari Nyekundu, Baisraeli balimushukuru kwa kumuimbia wimbo. (Kut 15:1-19) Banaume balianza kuimba ile wimbo ya mupya. (Kut 15:21) Yesu na Bakristo ba zamani balimusifu pia Yehova kwa kuimba. (Mt 26:30; Kol 3:16) Tunaendelea kuonyesha shukrani yetu kwa Yehova kwa kuimba ku mikutano na ku mikusanyiko. Kwa mufano, wimbo wenye tunatokea kuimba, “Aksanti Yehova,” unaimbiwaka ku mikutano tangu mwaka wa 1966.

Fasi ingine, banaume banasikiaka haya kuimba kati ya batu mingi. Bengine habaimbake juu banawazaka kama habana sauti ya muzuri. Lakini, tunapaswa kukumbuka kama kuimba ku mikutano yetu ni sehemu ya ibada. Tengenezo ya Yehova inajikaza sana juu ya kututolea nyimbo za muzuri na kuchagua nyimbo zenye tutaimba ku kila mukutano. Jambo yenye siye tunaweza kufanya tu ni kuimba pamoya na bengine juu ya kuonyesha shukrani yetu kwa Baba yetu wa mbinguni.

Muangalie VIDEO Tukumbuke Historia Yetu—Zawadi ya Wimbo, Sehemu ya 2. Kisha uliza wasikilizaji:

  • Kulitokea jambo gani ya pekee mu 1944?

  • Namna gani bandugu yetu ba mu Siberia balionyesha kama banapenda sana nyimbo za ufalme?

  • Juu ya nini Mashahidi wa Yehova wanaonaka kuimba kuwa jambo ya maana sana?

8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko

Maneno ya Kumalizia (Dak. 3) | Wimbo 73 na Sala