Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

“Heshimia Baba Yako na Mama Yako”

“Heshimia Baba Yako na Mama Yako”

Wakati Yesu alikuwa katika dunia alirudilia amri hii: ‘Umuheshimu baba yako na mama yako.’ (Kut 20:12; Mt 15:4) Ni wazi kama Yesu alikuwa na uhuru wa kusema kwa sababu aliendelea “kujitiisha” kwa wazazi wake wakati alikuwa kijana. (Lu 2:51) Wakati alikomaa, alifanya yake yote ili kisha Yeye kufa, mama yake atunzwe muzuri.​—Yoh 19:26, 27.

Leo pia, vijana Wakristo wanaonyesha wazazi wao heshima kwa kuwatii na kuzungumuza nao kwa heshima. Kwa kweli, amri ya kuheshimia wazazi wetu inatolewa kwa kila mutu. Hata wakati wazazi wamezeeka, tunapaswa kuendelea kuwaheshimia kwa kutafuta hekima kwao. (Met 23:22) Tunaonyesha pia kama tunaheshimia wazazi wenye kuzeeka kwa kuhangaikia mahitaji yao ya moyoni na ya feza. (1Tim 5:8) Vijana ao wazee, sisi wote tunapaswa kuendelea kuhangaikia wazazi wetu. Ni hivyo tutaonyesha kama tunawaheshimia.

MUANGALIE VIDEO NAMNA GANI NINAWEZA KUZUNGUMUZA NA WAZAZI WANGU? KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:

  • Sababu gani inaweza kuwa nguvu kwako kuzungumuza na wazazi wako?

  • Wakati unazungumuza na wazazi wako, namna gani unaweza kuwaonyesha heshima?

  • Sababu gani kuzungumuza na wazazi wako ni jambo lenye kufaa? (Met 15:22)

    Kuzungumuza na wazazi wako kunaweza kukusaidia ufanye maendeleo katika maisha