Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 14-15

Kulisha Watu Wengi Kupitia Wachache

Kulisha Watu Wengi Kupitia Wachache

Mbele tu ya Pasaka ya mwaka wa 32, Yesu alifanya muujiza. Ndiyo muujiza moja wenye Injili zote ine zinazungumuzia.

Kupitia muujiza huo, Yesu alianzisha njia yenye anaendelea kutumia mupaka leo.

14:16-21

  • Yesu aliomba wanafunzi wake wapatie kikundi cha watu chakula, hata kama walikuwa tu na mikate tano na samaki mbili

  • Yesu alikamata mikate na samaki, akasali, kisha akaanza kuigawia wanafunzi wake, nao wakaigawia kikundi cha watu

  • Kwa muujiza, chakula kikaongezeka na kila mutu akakula. Yesu alilisha maelfu ya watu kupitia wachache, ni kusema, wanafunzi wake

  • Yesu alisema kama katika siku za mwisho, atafanya njia ya kutoa ‘chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa.’​—Mt 24:45

  • Katika mwaka wa 1919, Yesu aliweka ‘mutumwa muaminifu na mwenye busara,’ kikundi kidogo cha ndugu watiwa-mafuta, juu ya “watumishi wake,” wale wenye kupewa chakula

  • Kupitia kikundi hicho kidogo cha ndugu watiwa-mafuta, Yesu anaendelea kufuata njia yenye alianzisha wakati wa mitume

Namna gani ninaweza kuonyesha kama ninakubali na kuheshimia njia yenye Yesu anatumia leo ili kutolea watu chakula cha kiroho?