MAISHA YA MUKRISTO
Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Tutumie Muzuri Maulizo
SABABU GANI NI LAZIMA: Ikiwa ‘mawazo katika moyo wa mutu ni kama kilindi cha maji,’ maulizo ni kama mbeketi ya kutusaidia kushota maji hayo. (Met 20:5) Maulizo inachochea wasikilizaji wetu watoe mawazo yao. Majibu ya maulizo yenye kuchaguliwa muzuri inaleta matokeo ya muzuri. Yesu alitumia muzuri maulizo. Namna gani tunaweza kumuiga?
NAMNA YA KUFANYA:
-
Uliza maulizo ya kuchochea mutu atoe mawazo yake. Yesu alitumia maulizo mbalimbali ili kujua mawazo ya wanafunzi wake. (Mt 16:13-16; be uku. 238 fu. 3-5) Unaweza kuuliza maulizo gani ya kuchochea mutu atoe mawazo yake?
-
Uliza maulizo ya kuongoza mutu. Ili kurekebisha mawazo ya Petro, Yesu alimuuliza maulizo na kutoa majibu mbalimbali yenye ilimusaidia Petro apate jibu la kweli. (Mt 17:24-26) Unaweza kuuliza maulizo gani ya kuongoza mutu ili kumusaidia apate jibu la kweli?
-
Umupongeze musikilizaji wako. Kisha mwandishi fulani ‘kujibu kwa kutumia akili,’ Yesu alimupongeza. (Mk 12:34) Namna gani unaweza kupongeza mutu mwenye anajibia ulizo?
MUANGALIE SEHEMU YA KWANZA YA VIDEO FANYA KAZI YENYE YESU ALIFANYA—FUNDISHA, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:
-
Hata kama ni habari za kweli, sababu gani huo ni mufano mubaya wa kufundisha?
-
Sababu gani hatupaswe tu kufasiria habari?
MUANGALIE SEHEMU YA PILI YA VIDEO HIYO, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:
-
Namna gani ndugu huyo alitumia muzuri maulizo?
-
Ni mambo gani ingine tunaweza kuiga katika namna yake ya kufundisha?