Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri​—Tutumie Muzuri Maulizo

Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri​—Tutumie Muzuri Maulizo

SABABU GANI NI LAZIMA: Ikiwa ‘mawazo katika moyo wa mutu ni kama kilindi cha maji,’ maulizo ni kama mbeketi ya kutusaidia kushota maji hayo. (Met 20:5) Maulizo inachochea wasikilizaji wetu watoe mawazo yao. Majibu ya maulizo yenye kuchaguliwa muzuri inaleta matokeo ya muzuri. Yesu alitumia muzuri maulizo. Namna gani tunaweza kumuiga?

NAMNA YA KUFANYA:

  • Uliza maulizo ya kuchochea mutu atoe mawazo yake. Yesu alitumia maulizo mbalimbali ili kujua mawazo ya wanafunzi wake. (Mt 16:13-16; be uku. 238 fu. 3-5) Unaweza kuuliza maulizo gani ya kuchochea mutu atoe mawazo yake?

  • Uliza maulizo ya kuongoza mutu. Ili kurekebisha mawazo ya Petro, Yesu alimuuliza maulizo na kutoa majibu mbalimbali yenye ilimusaidia Petro apate jibu la kweli. (Mt 17:24-26) Unaweza kuuliza maulizo gani ya kuongoza mutu ili kumusaidia apate jibu la kweli?

  • Umupongeze musikilizaji wako. Kisha mwandishi fulani ‘kujibu kwa kutumia akili,’ Yesu alimupongeza. (Mk 12:34) Namna gani unaweza kupongeza mutu mwenye anajibia ulizo?

MUANGALIE SEHEMU YA KWANZA YA VIDEO FANYA KAZI YENYE YESU ALIFANYA​—FUNDISHA, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:

  • Hata kama ni habari za kweli, sababu gani huo ni mufano mubaya wa kufundisha?

  • Sababu gani hatupaswe tu kufasiria habari?

MUANGALIE SEHEMU YA PILI YA VIDEO HIYO, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:

  • Namna gani ndugu huyo alitumia muzuri maulizo?

  • Ni mambo gani ingine tunaweza kuiga katika namna yake ya kufundisha?

Mafundisho yetu iko na matokeo gani juu ya wengine? (Lu 24:32)