Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 18-19

Epuka Kukwazika na Kukwaza Wengine

Epuka Kukwazika na Kukwaza Wengine

Yesu alitumia mifano ili kuonyesha hatari ya kukwazika ao ya kukwaza wengine.

18:6, 7

  • Hapa “kikwazo” ni tendo ao hali yenye inamupeleka mutu katika njia ya mubaya, ni kujikwaa ao kuanguka, ao ni kuangukia katika zambi

  • Ingekuwa muzuri zaidi kama wangefungia jiwe la kusagia kwenye shingo la mutu mwenye anakwaza mwengine na kumutupa ndani ya bahari

Jiwe la kusagia

18:8, 9

  • Yesu alishauri wanafunzi wake wakate kitu cha lazima sana kama vile mukono ao jicho kama kinafanya wakwazike

  • Ingekuwa muzuri zaidi kuachana na kitu cha lazima kama hicho ili kuingia katika Ufalme wa Mungu, kuliko kubakia nacho lakini kuishia katika Gehena, yenye kufananisha uharibifu wa milele

Katika maisha yangu, ni nini inaweza kuwa kikwazo, na namna gani ninaweza kuepuka kukwazika na kukwaza wengine?