Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 12-13

Mufano wa Ngano na Magugu

Mufano wa Ngano na Magugu

Yesu alitumia mufano wa ngano na magugu ili kuonyesha ni wakati gani na namna gani angeanza kuchagua na kukusanya jamii yote ya ngano ya Wakristo watiwa-mafuta; kazi ya kupanda ilianza katika mwaka wa 33.

13:24

‘Mutu alipanda mbegu ya muzuri katika shamba lake’

  • Mupandaji: Yesu Kristo

  • Mbegu ya muzuri inapandwa: Wanafunzi wa Yesu wanatiwa mafuta kwa roho takatifu

  • Shamba: Ulimwengu wa wanadamu

13:25

‘Wakati watu walikuwa wamelala usingizi, adui yake akakuja na kupanda magugu’

  • Adui: Shetani Ibilisi

  • Watu walikuwa wamelala: Kifo cha mitume

13:30

‘Muache zote zikomae pamoja mupaka wakati wa mavuno’

  • Ngano: Wakristo watiwa-mafuta

  • Magugu: Wakristo wa uongo

‘Mukusanye magugu kwanza . . . ; kisha mukusanye ngano’

  • Watumwa/​wavunaji: Malaika

  • Magugu yanakusanywa: Wakristo wa uongo wanatenganishwa na Wakristo wa kweli

  • Kukusanya na kutia katika depo: Wakristo watiwa-mafuta wanakusanywa katika kutaniko

Wakati mavuno ilianza, ni nini ilionyesha wazi tofauti kati ya Wakristo wa kweli na wa uongo?

Kuelewa maana ya mufano huo kunaniletea faida gani?