Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Tuwakaribishe Wageni Wetu

Tuwakaribishe Wageni Wetu

Siku ya 3, tarehe 23, Mwezi wa 3 tunangojea kupokea kwenye Ukumbusho wageni karibu milioni 12 ao zaidi. Ni ushahidi mukubwa sana wenye utatolewa na musemaji wakati atazungumuzia zawadi ya Yehova ya zabihu ya ukombozi na baraka fulani za wakati unaokuja zenye zabihu hiyo italetea wanadamu! (Isa 11:6-9; 35:5, 6; 65:21-23; Yoh 3:16) Hata hivyo, haiko tu musemaji ndiye atatoa ushahidi kwenye tukio hilo la pekee. Kila mutu anaweza kutoa ushahidi kwa kuwakaribisha wageni wetu kwa furaha. (Rom 15:7) Unaweza kufanya hivi:

  • Kuliko kukaa pa nafasi yako na kungoja mupaka programu ianze, ukaribishe kwa uchangamufu na kusalimia kwa furaha wageni na wale wenye hawakusanyike tena

  • Hata kama utahangaikia sana watu wenye ulialika, usisahau kuhangaikia pia wale wenye wamekuja kwa sababu walialikwa na ndugu na dada zetu wengine wakati wa kampanye. Uwaombe wakae pembeni yako. Utumie Biblia yako na kitabu chako cha wimbo pamoja nao

  • Kisha hotuba, ukuwe tayari kujibu maulizo yao. Kama wakati itakuwa kidogo kwa sababu munapaswa kuachia wengine nafasi, kamata mipango ili umutembelee pasipo kukawia. Kama haujue namna ya kumuona tena, unaweza kumuuliza hivi: “Ningependa kujua mawazo yako kuhusu mafundisho yenye tunatoka kufuata. Namna gani tunaweza kuonana tena?”