Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Namna ya Kutumia Broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?

Namna ya Kutumia Broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?

Broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo? imetayarishwa ili uichunguze pamoja na mwanafunzi wa Biblia, mbele ao kisha kila funzo. * Somo la 1 mupaka 4 zinasaidia wanafunzi wajue kama sisi ni watu wa namna gani, somo la 5 mupaka 14 zinawasaidia wajue kazi yetu, na somo la 15 mupaka 28 zinawasaidia wajue muzuri tengenezo letu. Kama somo fulani linazungumuzia jambo lenye kupatana na mambo munajifunza, munaweza kulichunguza; lakini ni muzuri zaidi kuchunguza somo namna zinafuatana katika broshua. Kila somo linachukua ukurasa moja, na mara nyingi wanafunzi wanalichunguza pamoja na walimu wao kwa dakika tano ao kumi.

  • Kazia uangalifu wa mwanafunzi kwenye ulizo kubwa lenye kuwa kichwa cha somo

  • Musome pamoja somo lote ao sehemu-sehemu

  • Muzungumuzie mambo yenye mumetoka kusoma. Tumia maulizo yenye kuwa kwenye mwisho wa ukurasa na muzungumuzie picha. Chagua maandiko yenye mutasoma. Onyesha namna vichwa vidogo-vidogo vinajibia ulizo kubwa ao kichwa cha somo

  • Kama somo liko na kisanduku “Ikiwa Unapenda Kujua Zaidi,” mukisome pamoja na utie moyo mwanafunzi atumikishe mashauri hayo

^ fu. 3 Broshua yenye kupatikana kwenye Internete ndio ya sasa.