Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Namna ya Kutumia Broshua Umusikilize Mungu

Namna ya Kutumia Broshua Umusikilize Mungu

Broshua Umusikilize Mungu imetayarishwa ili kusaidia watu wenye kuwa na magumu ya kusoma wajifunze kweli za musingi za Biblia kupitia picha. Kila somo linachukua kurasa mbili na linajaa picha zenye zimetayarishwa muzuri. Kuna alama za mukuki zenye kusaidia kujua namna picha hizo zinafuatana ili kuongoza mazungumuzo muzuri.

Broshua Umusikilize Mungu ili Uishi Milele iko na picha zile-zile zenye kupatikana katika broshua Umusikilize Mungu. Lakini, broshua Umusikilize Mungu ili Uishi Milele iko na maandishi mengi zaidi na ni ya kujifunza pamoja na wanafunzi wenye wanajua kusoma kidogo. Wahubiri wengi wanafurahia kuitumia wakati wanafunzi wao wanatumia Umusikilize Mungu. Kwenye mwisho wa kurasa nyingi kuna maneno fulani yenye munaweza kuzungumuzia kulingana na uwezo wa mwanafunzi.

Unaweza kumutolea mutu broshua moja kati ya hizo wakati wowote, hata kama haiko toleo la mwezi. Wakati unaongoza funzo la Biblia, tumia picha ili kueleza habari za Biblia. Uliza mwanafunzi maulizo ili alete mawazo yake na uhakikishe kwamba anaelewa. Musome na kuzungumuzia maandiko yenye kuwa kwenye mwisho wa kila kurasa. Kisha kumaliza broshua, muanze kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? ao kitabu Biblia Inaweza Kutufundisha Nini? [hakijapatikana katika Swahili (Congo)] ili kumusaidia mwanafunzi afikie ubatizo.