Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Saidia Familia Yako Imukumbuke Yehova

Saidia Familia Yako Imukumbuke Yehova

Yeremia alipewa mugao wa kutangazia Wayahudi uharibifu wenye ulikuwa karibu kutokea kwa sababu walikuwa wamemusahau Yehova, Mungu wao. (Yer 13:25) Namna gani taifa lilifikia hali hiyo ya mubaya kiroho? Familia za Waisraeli zilianza kuregea kiroho. Inaonekana kwamba, vichwa vya familia havikuwa vinafuata muongozo wa Yehova wenye kupatikana katika Kumbukumbu la Torati 6:5-7.

Leo, familia zenye kuwa nguvu kiroho zinafanya makutaniko yakuwe pia nguvu kiroho. Vichwa vya familia vinaweza kusaidia familia zao zimukumbuke Yehova kwa kufanya kwa ukawaida Ibada ya Familia yenye kujenga. (Zab 22:27) Kisha kuangalia video “Maneno Haya . . . Lazima Yawe Katika Moyo Wako”—Maelezo ya Familia, mujibie maulizo haya:

  • Namna gani familia fulani zimeweza kupiganisha matatizo yenye mara nyingi inavuruga ibada ya familia zao?

  • Familia hizo zimepata baraka gani?

  • Kuhusu ibada yangu ya familia, niko na matatizo gani, na namna gani naweza kupambana nayo?