Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Namna ya Kukomalisha Upendo Wetu kwa Mungu na kwa Jirani

Namna ya Kukomalisha Upendo Wetu kwa Mungu na kwa Jirani

Hata kama Wakristo hawafuate tena Sheria ya Musa, zile amri mbili kubwa zaidi za Sheria hiyo, ni kusema, kumupenda Mungu na kumupenda jirani, ni kifupi cha mambo yote yenye Yehova anatuomba. (Mt 22:37-39) Hatuzaliwe na upendo huo. Tunapaswa kuukomalisha. Namna gani? Moja kati ya njia za lazima zaidi ni kusoma Biblia kila siku. Wakati tunawaza sana juu ya sifa mbalimbali za Mungu zenye tunasoma katika Biblia, tunajionea “uzuri wa Yehova.” (Zab 27:4) Hilo linafanya upendo wetu kwake ukomae na tuanze kuona mambo kama yeye. Kwa kufanya hivyo, tunachochewa kutii amri za Mungu, kwa mufano amri ya kuonyesha wengine upendo wa kujizabihu. (Yoh 13:34, 35; 1Yoh 5:3) Mapendekezo haya tatu inaweza kutusaidia tufurahie zaidi usomaji wetu wa Biblia:

  • Tumia uwezo wako wa kufikiri, na hisia zako. Wazia kama uko hapo. Ona, sikia sauti, na harufu. Ujiulize: Watu wenye kuzungumuziwa walijisikia namna gani?

  • Badilisha namna yako ya kusoma. Mapendekezo fulani: Soma kwa sauti, ao sikiliza rekodi kwa kufuata katika Biblia yako. Kuliko kusoma sura namna zinafuatana, soma juu ya mutu ao habari fulani. Kwa mufano, ili kupata habari zaidi juu ya Yesu, tumia Nyongeza A7 ao B12 katika Biblia Takatifu​—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, ao sehemu ya 4 ao ya 16 ya broshua Musaada wa Kujifunza Neno la Mungu. Soma sura yote mwenye andiko la siku lilichukuliwa. Soma vitabu vya Biblia kufuatana na wakati viliandikwa.

  • Soma na kusudi la kuelewa. Ni muzuri zaidi kusoma hata sura moja kila siku na kuielewa na kufikiri sana, kuliko kusoma sura nyingi ili tu kumaliza habari zenye tunasoma. Chunguza ni katika hali gani habari iliandikwa. Chunguza hata mambo madogo-madogo. Tumia karte na michoro na pia maelezo ya pembeni ao ya katikati. Ujikaze kutafuta hata jambo moja lenye hauelewe. Kama inawezekana, tumia wakati uleule ili kuwaza sana juu ya mambo yenye unasoma.