Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 25

“Endelea Kukesha”

“Endelea Kukesha”

25:1-12

Hata kama mufano wa Yesu wa mabikira kumi ulihusu kwanza wanafunzi wake watiwa-mafuta, somo lenye kupatikana katika mufano huo linahusu Wakristo wote. (w15 15/3 uku. 12-16) ‘Kwa hiyo, muendelee kukesha kwa sababu hamuijue ile siku wala saa.’ (Mt 25:13) Unaweza kufasiria mufano huo wa Yesu?

  • Bwana-arusi (mustari wa 1)​—Yesu

  • Mabikira wenye busara, wenye kuwa tayari (mustari wa 2)​—Wakristo watiwa-mafuta wenye wako tayari kutimiza mugao wao kwa uaminifu na wenye wanaangaza kama mianga mupaka mwisho (Flp 2:15)

  • Sauti kubwa: “Bwana-arusi anafika!” (mustari wa 6)​—Alama ya kuwapo kwa Yesu

  • Mabikira wapumbavu (mustari wa 8)​—Wakristo watiwa-mafuta wenye wanatoka ili kukutana na Bwana-arusi lakini hawaendelee kukesha na wanakosa kuwa washikamanifu

  • Mabikira wenye busara wanakataa kupatia wengine mafuta yao (mustari wa 9)​—Kisha kutiwa muhuri kwa mara ya mwisho, watiwa-mafuta waaminifu hawatakuwa tena na wakati wa kusaidia watiwa-mafuta wenye walikosa kuwa waaminifu

  • “Bwana-arusi akafika” (mustari wa 10)​—Yesu anakuja kuleta hukumu karibu na mwisho wa ziki kubwa

  • Mabikira wenye busara wanaingia pamoja na bwana-arusi kwenye karamu ya ndoa, na mulango unafungwa (mustari wa 10)​—Yesu anakusanya watiwa-mafuta wake waaminifu mbinguni, lakini watiwa-mafuta wenye walikosa kuwa waaminifu wanapoteza zawadi yao ya kuenda mbinguni