Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri​—Tuonyeshe Wanafunzi Wetu Namna ya Kujitayarisha

Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri​—Tuonyeshe Wanafunzi Wetu Namna ya Kujitayarisha

SABABU GANI NI LAZIMA: Kama wanajitayarisha, wanafunzi wa Biblia wanaweza kuelewa muzuri zaidi na kukumbuka mambo yenye tunawafundisha. Kadiri wanaelewa na kukumbuka, watafanya maendeleo haraka. Hata kisha kubatizwa, wanapaswa kuendelea kujitayarisha kwa ajili ya mikutano na mahubiri ili ‘waendelee kukesha.’ (Mt 25:13) Kwa hiyo, kama wanajua namna ya kujifunza na kama wako na programe muzuri ya funzo, hilo litawaletea faida maisha yao yote. Tangu mwanzo, tunapaswa kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia wazoee kujitayarisha.

NAMNA YA KUFANYA:

  • Ukuwe mufano muzuri. (Rom 2:21) Fikiria mahitaji ya mwanafunzi wako kila mara wakati unajitayarisha. (km 11/15 uku. 3) Umuonyeshe namna umetayarisha katika kichapo chako

  • Umutie moyo ajitayarishe. Wakati funzo linaanza kabisa, umuonyeshe kama kujitayarisha ni sehemu ya funzo la Biblia, na umuonyeshe faida ya kujitayarisha. Umuonyeshe namna anaweza kupata wakati wa kujitayarisha. Wakati wa funzo, walimu fulani wanapatia mwanafunzi kichapo chao chenye wametayarisha muzuri ili kumusaidia aone faida ya kujitayarisha. Kama alijitayarisha, umupongeze

  • Umuonyeshe namna ya kujitayarisha. Wakati tu wanaanza kujifunza na mutu, walimu fulani wanatumia wakati wote wa funzo ili kumuonyesha namna ya kujitayarisha