Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri​—Namna ya Kuandika Barua

Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri​—Namna ya Kuandika Barua

SABABU GANI NI LAZIMA: Kitabu cha 1 Wakorinto ni moja kati ya barua 14 zenye mutume Paulo aliandikia Wakristo juu ya kuwatia moyo. Wakati mutu anaandika barua, anachaguaka kwa uangalifu maneno yenye ataandika, na mwenye atapokea ile barua anaweza kuisoma tena na tena. Tunaweza kutumia barua juu ya kuhubiria watu wa jamaa na marafiki. Barua inaweza pia kutusaidia kuhubiria watu wenye hatujapataka nafasi ya kuzungumuza nao uso kwa uso. Kwa mufano, pengine tulikutana na mutu fulani mwenye alipendezwa, lakini iko nguvu kumukuta kwake. Inaweza kuwa nguvu kuhubiria watu fulani wa eneo yetu juu wanaishi mu manyumba yenye kulindwa sana, mu lupango zenye watu hawaruhusiwe kuingia, ao mu maeneo ya mbali sana. Wakati unaandikia barua mutu mwenye haujue, ni mambo gani unapaswa kufikiria?

NAMNA YA KUFANYA:

  • Andika mambo yenye ungesema kama ungekutana naye uso kwa uso. Ujitambulishe ku mwanzo ya barua na uonyeshe waziwazi juu ya nini unaandika ile barua. Unaweza kuuliza ulizo yenye mutu atafikiria, na kumutuma ku site yetu. Kisha, umuambie kuhusu sehemu Masomo ya Biblia ku Enternete, uzungumuzie kwa kifupi namna tunajifunzaka na watu Biblia ku nyumba, ao utaje vichwa vya sura fulani za vichapo vyetu vya kutusaidia kujifunza Biblia na watu. Unaweza kutia ndani ya barua kichapo, karte ya jw.org, mwaliko, ao trakte

  • Usiandike mambo mingi. Usiandike barua ya murefu, juu mwenye unaandikia asichoke na kuacha kuisoma.​—Ona barua ya mufano

  • Soma barua yako juu uone kama haina makosa, na uhakikishe kama mawazo inapangiwa muzuri, kama inasomeka muzuri, kama ulitumia maneno ya kirafiki, kama haina maneno ya kukwaza, na kama haina maneno ya kuvunja moyo