Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri​—Kuhubiria Vipofu

Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri​—Kuhubiria Vipofu

JUU YA NINI NI JAMBO LA MAANA: Vipofu wengi hawapendake kuzungumuza na watu wenye hawajue. Kwa hiyo, inaomba kuwa na ufundi ili kuwahubiria. Yehova anahangaikiaka vipofu kwa upendo. (Law 19:14) Tunaweza kufuata mufano wake kwa kusaidia vipofu wajifunze juu ya Yehova.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • “Mutafute” vipofu. (Mt 10:11) Unajua watu fulani wenye kuwa na kipofu mu familia yao? Mu eneo lenu muko masomo ao nyumba kwenye vipofu wanaishi ao fasi zingine kwenye pengine watu wanaweza kupendezwa na vichapo vyenye vimetayarishwa kwa ajili ya vipofu?

  • Onyesha kama unawahangaikia kabisa. Wakati uko mwenye urafiki na wakati unaonyesha kama unamuangaikia kipofu, ile itafanya ajisikie kuwa mwenye kutulia. Jaribu kuanzisha mazungumuzo juu ya habari fulani yenye inafurahishaka watu mu eneo lenu

  • Uwapatie musaada wa kiroho. Katika tengenezo, tuko na vichapo vya aina mbalimbali vya kusaidia vipofu ao wale wenye hawaonake muzuri. Uulize mutu namna anapenda kujifunza. Mwangalizi wa utumishi anapaswa kuhakikisha kama mutumishi wa vichapo anajaza maombi ya vichapo vya aina yenye vipofu wanapenda.