Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Nitaalika Nani?

Nitaalika Nani?

Kila mwaka tunajikaza sana kualika watu wa eneo letu ili wakuje kuhuzuria Ukumbusho pamoja na sisi. Wengi kati yao hatuwajue. Tunapaswa pia kualika watu wenye tunajua. Mara mingi watu wenye wanapewa mualiko na watu wenye wanajua, inawezekana wakuje kuhuzuria. (yb08 uku. 11 fu. 3; uku. 14 fu. 1) Ni nani unaweza kualika?

  • Watu wa jamaa yako

  • Wafanyakazi wenzako ao wanafunzi wenzako

  • Majirani wako

  • Watu wenye utarudilia na mafunzo yako ya Biblia ya zamani na ya sasa

Tena, wazee wataalika wale wenye hawahubiri tena. Utafanya nini kama mutu mwenye unajua haishi katika eneo lenu? Unaweza kupata saa na mahali kwenye Ukumbusho utafanyika katika eneo lake kwa kufungua sehemu yenye kichwa HABARI JUU YETU, yenye kuwa kwenye sehemu ya juu ya ukurasa wa mwanzo wa jw.org, na ufungue sehemu “Ukumbusho.” Wakati unajitayarisha kwa ajili ya Ukumbusho wa mwaka huu, fikiria ni nani unaweza kualika, na kisha umupatie mualiko.